Connect with us

Magonjwa

je kutokwa na uchafu mweupe ukeni ni ugonjwa

Avatar photo

Published

on

je kutokwa na uchafu mweupe ukeni ni ugonjwa

Uchafu mweupe ukeni ukitoka na rangi nyeupe, kuonekana vizuri, pasipo na harufu ni kawaida, Ingawa mabadiliko haya huweza kuashiria tatizo;

  • Kutoka Mwingi
  • Kutoka mfululizo
  • Kubadilika rangi
  • Kuwa na harufu n.k

Uchafu Mweupe Ukeni(Clear or white):

Uchafu mweupe Ukeni ukiwa Mzito na kuambatana na harufu pamoja na miwasho huweza kuashiria maambukizi kama vile ya Fangasi(yeast infection).

NB: Kutokwa na uchafu ukeni hutokea kwa kawaida katika mzunguko wako wa hedhi. Baadhi ya mabadiliko katika kutokwa na uchafu ukeni yanaweza kutokea kutokana na hali fulani za matibabu, au maambukizi ya magonjwa kama vile fangasi.

Fahamu ni Majimaji ambayo husaidia kuweka uke safi na bila maambukizi, kutokwa na uchafu mweupe ukeni ni asili kabisa. Lakini rangi yake, kiwango au kiasi chake kinaweza kutofautiana, ikitegemea umri wako na mahali ulipo katika mzunguko wako wa hedhi.

Mabadiliko kadhaa, hata hivyo, yanaweza kuwa ishara ya hali ya kiafya. Haya yanaweza kujumuisha mabadiliko makubwa ya rangi au harufu pamoja na tofauti ya uwiano.

Ni vizuri Zaidi kufanya uchunguzi Kuanzia aina na sababu hadi wakati Uchafu mweupe ukeni unatoka, ili ikiwa kuna tatizo lolote au mabadiliko yoyote ufahamu mapema na kutafta Msaada wa kitaalam.

Aina za Uchafu Ukeni

Hizi ni aina Mbali mbali za uchafu Ukeni, Aina hizi mara nyingi huwekwa kulingana na rangi;

(1) Uchafu Mweupe Ukeni(White)

Kutokwa na Uchafu Mweupe ukeni ni kawaida, na mara nyingi hutokea hasa karibu na wakati wa kuanza kwa mzunguko wa hedhi au mwishoni mwa mzunguko wa hedhi.

Kawaida ya Uchafu huu ni kuwa mweupe, wenye kuvutika lakini usio na harufu mbaya.

(2) Uchafu mweupe mwithili ya maji(Clear and watery)

Karibu na kipindi cha yai kutoka(ovulation), Unaweza kupata uchafu mweupe wenye kuvutika Zaidi, na unafanana kabsa na ule ambao mwanamke akisisimka zaidi kihisia wakati wa kufanya mapenzi hutoka, Au hata wakati wa Ujauzito.

(3) Uchafu wa Brown au Nyekundu(bloody)

Kutokwa na uchafu wa kahawia au kama damu kunaweza kutokea wakati au mara baada ya mzunguko wako wa hedhi. Unaweza pia kupata kutokwa na damu kidogo kati ya hedhi. Hii inaitwa spotting.

Kutokwa na Uchafu kunakotokea wakati wa kawaida wa kipindi chako cha hedhi na baada ya kufanya ngono huweza kuwa na Ishara kiafya.

Na kutokwa na damu mapema kunaweza kuwa ishara ya kuharibika kwa mimba ikiwa wewe ni mjamzito.

(4) Uchafu wa Njano au kijani(Yellow or green)

Kutokwa na uchafu ukeni wa manjano au kijani kibichi zaidi – haswa ikiwa ni Mzito, na ukiambatana na harufu mbaya- ni ishara ya tatizo kiafya, hivo hakikisha unapata msaada kutoka kwa mtaalamu wa afya.

Chanzo cha Kutokwa na Uchafu Ukeni

Kutokwa na uchafu ukeni ni utendaji mzuri wa mwili unaotokana na mabadiliko ya asili katika viwango vya vichocheo aina ya estrojeni. Kiasi cha kutokwa na majimaji au uchafu ukeni kinaweza kuongezeka kutokana na kuwa kwenye kipindi cha yai kutoka(ovulation), msisimko wakati wa kufanya mapenzi, matumizi ya vidonge vya kudhibiti uzazi, na ujauzito.

Rangi, harufu na mwonekano wa uchafu unaotoka ukeni unaweza kuathiriwa vibaya na mabadiliko ya usawa wa bakteria wa ukeni. Hiyo ni kwa sababu idadi ya bakteria hatari inapoongezeka, maambukizo kwenye uke yanawezekana zaidi.

Hapa kuna baadhi ya maambukizi yanayoweza kupelekea shida hii ya Kutokwa na Uchafu Ukeni;

– Maambukizi ya bacteria(Bacterial vaginosis)

Bacterial vaginosis ni maambukizi ya bakteria, maambukizi haya Husababisha kuongezeka kwa uchafu kutoka ukeni ambao una harufu kali,  na wakati mwingine kuwa na harufu kama shombo ya samaki.

Kutokwa na uchafu kunaweza pia kuonekana kwa rangi ya kijivu, mwembamba, na majimaji. Na Katika hali nyingine, maambukizi haya hayatoi dalili zozote.

Ingawa ugonjwa wa bakteria vaginosis hauambukizwi kupitia mawasiliano ya ngono, una hatari kubwa ya kuupata ikiwa unafanya ngono au umepata mwenzi mpya hivi karibuni. Maambukizi yanaweza pia kukuweka kwenye hatari kubwa zaidi ya kuambukizwa magonjwa ya zinaa (STI).

– Trichomoniasis

Trichomoniasis ni aina nyingine ya maambukizi ambayo chanzo chake ni parasite.

Kawaida huenezwa kwa mawasiliano ya ngono(huu ni ugonjwa wa Zinaa), lakini pia unaweza kuambukizwa kwa kutumia taulo au nguo za kuoga.

Nusu ya watu walioathiriwa hawana dalili zozote. Lakini kwa Wale wenye dalili mara nyingi wataona kutokwa na uchafu wa njano, kijani, au povu na harufu isiyofaa. Maumivu, kuvimba na kuwasha kuzunguka uke na vilevile wakati wa kukojoa au kufanya ngono pia ni dalili za kawaida.

– Maambukizi ya Fangasi(Yeast infection)

Maambukizi ya Fangasi hutokea wakati ukuaji wa fangasi unapoongezeka kwenye uke. Husababisha kutokwa na uchafu mzito kama maziwa ya mtindi na mweupe unaofanana na jibini.

Dalili zingine ni pamoja na kuwashwa karibu na uke pamoja na maumivu wakati wa tendo au wakati wa kukojoa.

Yafuatayo yanaweza kuongeza uwezekano wa kupata maambukizi Zaidi ya Fangasi sehemu za Siri;

– kuwa na Msongo wa  mawazo(stress)

– Ugonjwa wa kisukari

– matumizi ya dawa za kupanga uzazi

– Kuwa na mimba

– Matumizi ya antibiotics, hasa matumizi ya muda mrefu zaidi ya siku 10 n.k

– Ugonjwa wa kisonono na Pangusa(Gonorrhea and chlamydia)

Kisonono na chlamydia ni magonjwa ya zinaa ambayo yanaweza kusababisha kutokwa na uchafu ukeni usio wa kawaida kutokana na kuambukiza eneo la seviksi. Mara nyingi huwa na rangi ya manjano, kijani kibichi au mawingu.

Unaweza pia kupata:

  • maumivu wakati wa kukojoa
  • maumivu ya tumbo
  • kutokwa na damu ukeni baada ya kujamiiana
  • kutokwa damu katikati ya mzunguko wa hedhi

Lakini watu wengine wanaweza pia wasionyeshe dalili zozote.

– Genital herpes

Ugonjwa huu ni miongoni mwa magonjwa ya zinaa yanayoweza kusababisha kutokwa na uchafu mzito ukeni huku kukiwa na harufu kali, hasa baada ya kufanya mapenzi.

Vidonda na malengelenge yanaweza kutokea sehemu za siri pamoja na kutokwa na damu katikati ya mzunguko wa hedhi na kupata hisia ya kuwaka moto wakati wa kukojoa.

– Ugonjwa wa PID(Pelvic inflammatory disease)

Kutokwa na uchafu mwingi na harufu mbaya pamoja na maumivu ndani ya tumbo, baada ya ngono, au wakati wa hedhi au kukojoa kunaweza kuwa dalili za ugonjwa wa maambukizi ya bacteria kwenye via vya uzazi vya mwanamke(PID).

Hii hutokea wakati bakteria Kuingia kwenye uke na kufika hadi kwenye viungo vingine vya uzazi na inaweza kusababishwa na magonjwa ya zinaa ambayo yameachwa bila kutibiwa kama vile klamidia au kisonono.

– Maambukizi ya HPV au Saratani ya Shingo ya Kizazi(Human papillomavirus or cervical cancer)

Maambukizi ya virusi vya Human papilloma(HPV) huenezwa kwa njia ya ngono na yanaweza kusababisha saratani ya shingo ya kizazi. Ingawa kunaweza kuwa hakuna dalili, aina hii ya saratani inaweza kusababisha:

  • kutokwa na damu, Uchafu wa kahawia, au majimaji yenye harufu mbaya ukeni
  • kutokwa na damu isiyo ya kawaida katikati ya mzunguko wa hedhi au baada ya kujamiiana
  • maumivu wakati wa kukojoa au kuongezeka kwa hamu ya kukojoa

Katika hali ya nadra, kutokwa na majimaji ya hudhurungi au damu kunaweza pia kuwa ishara ya saratani ya endometriamu, fibroids, au ukuaji mwingine wa seli.

Ikiwa una dalili za Matatizo haya, hakikisha unapata matibabu.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa4 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa1 month ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa2 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa2 days ago

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi Madhara ya kula nyama ya ng’ombe mbichi Ni desturi ya baadhi ya watu kula...

Magonjwa1 week ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa3 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa4 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...