Connect with us

Magonjwa

Gangrene ni ugonjwa gani,au gangrene ni nini?

Avatar photo

Published

on

Gangrene ni ugonjwa gani,au gangrene ni nini?

Gangrene ni tatizo linalohusisha  kufa kwa tissu za mwili kutokana na kupungua kwa mtiririko wa damu au maambukizi makali.

Mara nyingi tatizo la gangrene huathiri mikono na miguu, ikiwa ni pamoja na vidole vya mikono na vidole vya miguu. Inaweza pia kutokea katika misuli na viungo vya ndani ya mwili, kama vile kwenye kifuko cha nyongo(gallbladder).

Hali yoyote inasababisha uharibifu wa mishipa ya damu, na kuathiri mtiririko wa damu(Blood flow),mfano ugonjwa wa kisukari, tatizo la mishipa ya arteries kuwa migumu”hardened arteries (atherosclerosis),n.k, vyote hivi huongeza hatari ya mtu kupata tatizo la gangrene.

gangrene ni tatizo ambalo linawapata Sana wagonjwa wa kisukari, husababisha sehemu ya mwili kubadilika rangi na tissues za sehemu hiyo kufa kutokana na mzunguko wa damu kutokufika sehemu hiyo,

Tatizo hili husambaa kwa haraka kwenye viungo vya mwili na lisipo tibiwa kwa haraka hupelekea mgonjwa kukatwa viungo na muda mwingine kusababisha kifo,

Tatizo hili linatibika katika hatua za awali hivyo ukimuona mgonjwa wa kisukari kaanza kuonesha dalili hizi wahi mapema hospital ili umsaidie kupata suluhisho.

Matibabu ya gangrene yanaweza kujumuisha dawa jamii ya antibiotics, tiba ya oksijeni, na upasuaji wa kurejesha mtiririko wa damu na kuondoa tishu zilizokufa. Gangrene ikitambuliwa mapema na kutibiwa, ndivyo uwezekano wa kupona huongezeka.

Dalili za tatizo la Gangrene

Ikiwa gangrene imeathiri ngozi,dalili zake ni pamoja na:

  1. Ngozi kubadilika rangi-kuanzia kijivu iliyokolea hadi bluu, zambarau, nyeusi, shaba au nyekundu
  2. Kuvimba eneo husika
  3. Kuwa na kama malengelenge
  4. Ghafla, kuanza kupata maumivu makali ikifuatiwa na kuhisi kufa ganzi
  5. Kutokwa na Uchafu wenye harufu mbaya kwenye kidonda
  6. Ngozi kuwa nyembamba, inayong’aa, au ngozi isiyo na nywele
  7. Kuhisi baridi kwenye Ngozi au baridi kwa kugusa
  8. Iwapo gangrene itaathiri tishu zilizopo chini ya ngozi yako, unaweza pia kuwa na homa ya kiwango cha chini na kwa ujumla kujisikia vibaya.

Gangrene kutokana na maambukizi makali, Ikiwa vijidudu vilivyosababisha gangrene vitaenea kupitia mwili, hali inayoitwa septic shock inaweza kutokea. Ishara na dalili za septic shock zinazoweza kutokea ni pamoja na:

– Kushuka kwa shinikizo la Damu(Low blood pressure)

– Kupata homa

– Mapigo ya moyo kwenda mbio

– Hali ya kukosa pumzi au kupumua kwa shida n.k

Chanzo cha tatizo la Gangrene

Sababu za kutokea kwa Gangrene ni pamoja na;

– Ukosefu wa usambazaji wa damu(Lack of blood supply)

Damu hubeba oksijeni na virutubisho kwenye mwili. Pia hutoa mfumo wa kinga na antibodies kupambana na maambukizi. Bila ugavi sahihi wa damu, seli haziwezi kuishi, na tishu hufa.

– Maambukizi ya magonjwa

Maambukizi ya vimelea kama bacteria ikiwa hayajatibiwa huweza kupelekea kupata tatizo la gangrene.

– Kuumia au kupata majeraha(Traumatic injury).

Majeraha ya risasi au majeraha ya kusagwa kutokana na ajali za gari n.k yanaweza kusababisha majeraha wazi ambayo huruhusu bakteria kuingia kwenye mwili. Ikiwa bakteria huambukiza tishu na kubaki bila kutibiwa, gangrene inaweza kutokea.

Vitu ambavyo huongeza hatari ya kupata Gangrene

  • Ugonjwa wa kisukari; Viwango vya juu vya sukari kwenye damu vinaweza hatimaye kuharibu mishipa ya damu. Uharibifu wa mishipa ya damu unaweza kupunguza au kuzuia mtiririko wa damu kwenye sehemu ya mwili ikiwemo kwenye tishu, na hii huweza kupelekea kutokea kwa gangrene.
  • Ugonjwa kwenye mishipa ya damu kama vile;(atherosclerosis),damu kuganda n.k
  • Kuumia sana au kupata majeraha
  • Upasuaji
  • Uvutaji wa Sigara
  • Unene kupita kiasi au Uzito mkubwa kupita kiasi
  • Kuwa na hali yoyote inayoshusha kinga ya mwili(Immunosuppression) kama vile;, huduma ya Chemotherapy, mionzi,baadhi ya maambukizi kama vile ya UKIMWI n.k

Madhara ya Gangrene:

Tatizo la gangrene linaweza kusababisha matatizo makubwa ikiwa hautatibiwa mara moja. Bakteria wanaweza kuenea haraka kwenye tishu na viungo vingine. Huenda ukahitaji kuondolewa sehemu ya mwili (kukatwa) ili kuokoa maisha yako.

Kuondolewa kwa tishu zilizoambukizwa kunaweza kusababisha kovu au hitaji la upasuaji wa kurekebisha.

Jinsi ya kuzuia au kujikinga na tatizo la Gangrene

Hapa kuna njia chache za kusaidia kupunguza hatari ya kupata tatizo la gangrene:

✓ Hakikisha unadhibiti Sukari yako

✓ Kama una maambukizi yoyote, hakikisha unapata tiba

✓ Kama una Jeraha au kidonda, hakikisha unapata matibabu na kupona haraka

✓ Dhibiti Uzito wako wa Mwili

✓ Epuka kuvuta Sigara au kutumia tumbaku n.k

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Ushauri|Tiba|CheckIn 🩺🌡️ContactUs; +255758286584 or INBOX📩. For More Healthtips everyday Link In https://afyaclass.com Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa4 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa1 month ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa2 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa2 days ago

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi Madhara ya kula nyama ya ng’ombe mbichi Ni desturi ya baadhi ya watu kula...

Magonjwa1 week ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa3 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa4 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...