Connect with us

magonjwa ya wanawake

CHANZO CHA TATIZO LA MASHAVU YA UKE KUWA MAREFU KULIKO KAWAIDA

Doctor Ombeni

Published

on

115 Views
0 Comments

 CHANZO CHA TATIZO LA MASHAVU YA UKE KUWA MAREFU KULIKO KAWAIDA

Hili ni tatizo ambalo huhusisha mashavu ya uke kuwa makubwa zaidi kuliko kawaida au kuongezeka ukubwa, na huwapata baadhi ya Wanawake,kwa kitaalam tatizo hili hujulikana kama Labial Hypertrophy,

ambapo huhusisha mashavu ya uke kukuwa na kuongezeka ukubwa,hapa nina maana ya Labia majora,na labial Minora,vyote kwa pamoja.

DALILI ZA TATIZO HILI LA MASHAVU YA UKE KUWA MAREFU KULIKO KAWAIDA

– Kama hakuna ukuaji mkubwa zaidi au ongezeko kubwa zaidi,ni vigumu sana mwanamke kupata dalili zozote za tofauti, ila kama mashavu ya uke yamekuwa makubwa zaidi,mwanamke huweza kupata dalili kama hizi hapa chini;

• Mwanamke Kuona hali ya kutuna kuliko kawaida kwa nguo akiwa amevaa hasa nguo zake za ndani

• Kupata shida ya kujisafisha maeneo ya ukeni, hii hutokea baada ya mwanamke kupata hisia kali akishika maeneo haya,hivo kuyakwepa,

hali ambayo hupelekea uchafu kujificha kwenye mikunjo hasa wakati wa period au hedhi,hali ambayo huweza kusababisha mwanamke kupatwa na maambukizi ya magonjwa yasioisha

• Hali ya kutekenywa ukeni, hii hutokea endapo mashavu ya uke yamekuwa makubwa zaidi, ambapo hupelekea msuguano mpaka kwenye nguo yako ya ndani hasa wakati wa kutembea,na wakati mwingine hupelekea hali ya miwasho pia

• Mwanamke kutokuwa comfortable wakati wa shughuli mbali mbali kama vile wakati wa kuendesha baiskeli,kupanda farasi n.k pamoja na kupata maumivu wakati wa tendo la ndoa

CHANZO CHA TATIZO HILI LA MASHAVU YA UKE KUONGEZEKA UKUBWA

Mpaka sasa Hakuna sababu ya moja kwa moja ambayo hujulikana ya kutokea kwa shida hii,ila kuna baadhi ya sababu zimeonekana kuongeza uwezekano wa kutokea kwa tatizo hili kwa baadhi ya Wanawake kama vile;

1. Tatizo la kigenetics,ambapo mwanamke huzaliwa tayari akiwa na shida hii

2. Hali ya vichocheo vya Estrogen pamoja na vichocheo vingine au hormones zingine za kike ambazo huzalishwa kwa kiwango kikubwa zaidi wakati wa balehe

3. Wakati wa Ujauzito,ambapo Mtiririko wa Damu(Blood flow) huwa mkubwa zaidi kuelekea maeneo ya via vya uzazi ikiwemo ukeni,

Hii huweza kuongeza presha na kusababisha shida hii

4. Mwanamke kupatwa na majeraha au ajali ambazo huhusisha kuumia kwenye mashavu ya ukeni

5. Na wakati mwingine baadhi ya maambukizi ya magonjwa sehemu za siri kama vile Fangasi,Magonjwa ya zinaa n.k huweza kuchangia Mwanamke kupatwa na tatizo hili la Mashavu ya uke kuwa makubwa kuliko kawaida.

MATIBABU YA TATIZO LA MASHAVU YA UKE KUWA MAKUBWA KULIKO KAWAIDA

– Matibabu hutegemea na chanzo husika Pamoja na ukubwa wa tatizo hili,ila kwa ujumla wake kuna matibabu ambayo huweza kuhusisha matumizi ya dawa mbali mbali Pamoja na huduma ya upasuaji ambayo kwa kitaalam hujulikana kama LABIOPLASTY.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

115 Views
0 Comments

Medical Disclaimer

Medical Disclaimer: Taarifa kwenye makala hii ni kwa ajili ya Updates au elimu ya jumla tu na haichukui nafasi ya uchunguzi,Tiba au ushauri wa kitaalamu wa daktari kwa mtu mmoja mmoja. Kama una dharura au tatizo lolote la kiafya, tafadhali Wasiliana na Daktari moja kwa moja hapa.

Je, unahitaji ushauri binafsi au matibabu ya tatizo lolote?

💬 Wasiliana na Daktari Hapa

🏆Certified| Doctor from Afyaclass. Maudhui haya ni kwa ajili ya elimu ya jumla ya afya. Unapohitaji ushauri wa kina, uchunguzi, au matibabu binafsi, wasiliana na daktari kupitia namba:+255758286584.Pia tufwatilie kupitia: @Facebook | @Instagram | @YouTube.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Guest Avatar

LATEST POSTS

magonjwa ya wanawake5 years ago

PID NI NINI? Na Dalili zake ni Zipi?(magonjwa ya Wanawake)

 PID • • • • • PID NI NINI? Na Dalili zake ni Zipi?(magonjwa ya Wanawake) PID NI NINI?  PID...

afyatips19 hours ago

Dalili za kidonda cha operation kupona

DALILI ZA KIDONDA CHA OPERATION KUPONA Baada ya kufanyiwa operation, mwili huanza mchakato wa kuponya kidonda mara moja. Mchakato huu...

Utafiti21 hours ago

Desogestrel yahusishwa na Kuongezeka kwa Hatari ya uvimbe wa ubongo

Mamlaka ya Dawa na Bidhaa za Afya ya Ufaransa (ANSM) imewaonya wanawake wanaotumia baadhi ya njia za uzazi wa mpango...

magonjwa5 years ago

UGONJWA WA BRUCELLA(chanzo,dalili na tiba)

UGONJWA WA BRUCELLA(chanzo,dalili na tiba) Huu ni ugonjwa ambao kwa kitaalam hujulikana kama brucellosis na chanzo chake ni bacteria wanaojulikana...

magonjwa ya watoto2 years ago

Ugonjwa wa Surua kwa Watoto: Sababu, Dalili, Matibabu na Kinga

Ugonjwa wa Surua kwa Watoto: Sababu, Dalili, Matibabu na Kinga Ugonjwa wa Surua ni ugonjwa wa kuambukiza sana kwa watoto...

Afya News2 days ago

Vifo vya Watoto Wachanga Katika Mlipuko wa Surua Pennsylvania na Mjadala wa Afya ya Umma

Mlipuko wa ugonjwa wa surua (measles) unaoendelea katika jimbo la Pennsylvania, Marekani, umeendelea kuzua wasiwasi mkubwa baada ya watoto wawili...

Afya News2 days ago

Wauguzi Kenya Wasitisha Mgomo Baada ya Makubaliano na Serikali

Wauguzi nchini Kenya wamesitisha mgomo wao wa siku 43 baada ya kufikia makubaliano na serikali kupitia chama chao cha wafanyakazi....

WHO3 days ago

Uvutaji Sigara Unaongeza Uwezekano wa Ugumba

Uvutaji Sigara Unaongeza Uwezekano wa Ugumba Shirika la Afya Duniani (WHO) limeonya kuwa matumizi ya tumbaku yana athari kubwa kwa...

magonjwa ya wanaume1 year ago

Dalili za Gono Sugu kwa Mwanaume (Gonorrhea sugu)

Gono sugu ni maambukizi ya zinaa yanayosababishwa na bakteria aitwaye Neisseria gonorrhoeae, ambayo yamekuwa yakujirudia rudia na hayaponi kwa baadhi...

Uzazi/Ujauzito4 days ago

Madhara ya Sindano ya depo,Fahamu hapa

Madhara ya Sindano ya Depo (Depot Medroxyprogesterone Acetate – DMPA) Sindano ya Depo-Provera (Depot Medroxyprogesterone Acetate – DMPA) ni mojawapo...

116
0