Connect with us

magonjwa ya wanawake

Ndizi 1 tu husaidia kupunguza na kuondoa Maumivu wakati wa Hedhi

Doctor Ombeni

Published

on

240 Views
0 Comments

Kwa Mwanamke anayepata maumivu makali wakati wa hedhi anaelewa jinsi maumivu hayo yanavyokuwa. Sasa hapa kuna kitu rahisi ambacho kinaweza kusaidia kidogo – ndizi.

Ndizi zina magnesiamu na vitamini B6, ambazo zote zina jukumu la kulegeza misuli na kupunguza Mkazo. Maumivu ya hedhi hutokea kwa sababu uterasi yako inasisimka na kubana zaidi(Contracts) ili kutoa utando wake. Magnesiamu husaidia kulegeza misuli laini, ambayo inaweza kupunguza nguvu ya mikazo hiyo. Utafiti fulani pia unaonyesha kwamba viwango vya kutosha vya magnesiamu vinaweza kupunguza prostaglandini -ambayo husababisha maumivu yanayoambatana na mikazo.

Hivi ndivyo ndizi inavyoweza kukusaidia wakati wa hedhi:

• Magnesiamu ndani yake husaidia kulegeza misuli ya uterasi

• Vitamini B6 inaweza kupunguza uvimbe,Mkazo na mabadiliko ya hisia

• Sukari asilia hutoa nishati ya haraka ikiwa unahisi dhaifu sana mwilini

• Potasiamu husaidia kuzuia maumivu ya misuli na uchovu

Ndizi moja haitaondoa kabsa maumivu makali, lakini inaweza kuwa msaada wa kupunguza maumivu na wa asili kama sehemu ya lishe bora kwa ujumla.

 Kwa matokeo bora, changanya na:

• Kunywa maji Vizuri,Uji au maziwa,Tangawizi,Maji ya uvuguvugu n.k.

• Kufanya mazoezi mapesi kama kujinyoosha au kutembea

• Kutumia Warm compress kwenye tumbo la chini

• Kulala vya kutosha n.k.

Kumbuka: Ikiwa maumivu yako ya hedhi ni makali, Hali inazidi kuwa mbaya, au yanaathiri maisha yako ya kila siku, ni muhimu kushauriana na mtaalamu wa afya. Hali kama vile endometriosis au PCOS zinahitaji mwongozo sahihi wa kimatibabu. Na Kwa ushauri zaidi unaweza kutuma Neno Afyaclass Inbox.

240 Views
0 Comments

Medical Disclaimer

Medical Disclaimer: Taarifa kwenye makala hii ni kwa ajili ya Updates au elimu ya jumla tu na haichukui nafasi ya uchunguzi,Tiba au ushauri wa kitaalamu wa daktari kwa mtu mmoja mmoja. Kama una dharura au tatizo lolote la kiafya, tafadhali Wasiliana na Daktari moja kwa moja hapa.

Je, unahitaji ushauri binafsi au matibabu ya tatizo lolote?

💬 Wasiliana na Daktari Hapa

🏆Certified| Doctor from Afyaclass. Maudhui haya ni kwa ajili ya elimu ya jumla ya afya. Unapohitaji ushauri wa kina, uchunguzi, au matibabu binafsi, wasiliana na daktari kupitia namba:+255758286584.Pia tufwatilie kupitia: @Facebook | @Instagram | @YouTube.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Guest Avatar

LATEST POSTS

Hospital8 hours ago

MNH-Mloganzila Yafanya Upasuaji wa Kurekebisha na Kurefusha Mifupa kwa Mbinu ya Ilizarov

MNH-Mloganzila Yafanya Upasuaji wa Kurekebisha na Kurefusha Mifupa kwa Mbinu ya Ilizarov Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH)-Mloganzila imefanikiwa kufanya kwa...

EVENTS9 hours ago

Wavunja Record ya Dunia kwa kupanda miche 2,51,446 kwa saa moja tu

Wavunja Record ya Dunia kwa kupanda miche 2,51,446 kwa saa moja tu. Katika juhudi kubwa za kushangaza kwenye kutunza mazingira,...

magonjwa ya wanawake11 hours ago

Fangasi Ukeni: Chanzo na Dalili

Fangasi Ukeni: Chanzo na Dalili Fangasi ukeni ni maambukizi ya fangasi yanayotokea kwenye uke na mara nyingi husababishwa na fangasi...

magonjwa ya wanawake1 day ago

Hedhi yenye harufu mbaya: SABABU zinazoweza kusababisha

Kwa baadhi ya wanawake, damu ya hedhi inaweza kuwa na harufu fulani ambayo si sawa na harufu ya kawaida ya...

EVENTS1 day ago

Siku ya kuzuia kujiua duniani 2026: kubadili mtazamo na kuanza mazungumzo

SIKU YA KUZUIA KUJIUA DUNIANI 2026: KUBADILI MTAZAMO NA KUANZA MAZUNGUMZO Kaulimbiu ya 2026: “Changing the Narrative on Suicide” –...

Utafiti1 day ago

Vifo Vinavyotokana na Mimba kutunga Nje ya Kizazi

Mimba kutunga nje ya kizazi (ectopic pregnancy) ni hali ambayo mimba inajipandikiza nje ya sehemu ya kawaida ya kizazi,Mara nyingi...

Utafiti2 days ago

Ucheleweshaji wa huduma Ndani ya Hospitali Wawa Tishio Kubwa kwa Maisha ya Mama na Mtoto

Ucheleweshaji wa huduma ndani ya vituo vya afya umeonekana kuwa moja ya sababu kubwa zinazochangia vifo vya wajawazito na watoto...

Afya News2 days ago

Jinsi Dawa za Kulevya Zinavyoharibu Afya ya Kinywa na Meno

Matumizi ya dawa za kulevya yanaweza kuathiri sehemu mbalimbali za mwili, ikiwemo ubongo, moyo, ini na mfumo wa fahamu. Hata...

magonjwa3 days ago

Ugonjwa wa Selimundu,dalili,chanzo na Tiba

Katika Makala hii tunachambua Zaidi kuhusu Dalili za ugonjwa wa seli mundu,chanzo cha ugonjwa wa Seli mundu pamoja na Matibabu...

Afya News3 days ago

Wataalam wa maabara wahimizwa kuboresha huduma za afya kwa Wananchi

WATAALAM WA MAABARA WAHIMIZWA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA KWA WANANCHI Na Zakayo Mosha- WAF Morogoro Wataalam wa Maabara wamehimizwa kutumia...

241
0