Afya News
UK yaidhinisha wagonjwa mahututi kupewa Msaada wa kujitoa Uhai
Wabunge wa Uingereza wameuidhinisha muswada wa sheria ya kuwaruhusu wagonjwa mahututi na ambao ni watu wazima kupewa msaada wa kumaliza uhai wao.
Baada ya miezi kadhaa ya majadiliano makali, muswada huo umefanikiwa kuvuuka kihunzi cha kwanza hivi leo kabla ya kuidhinishwa rasmi kuwa sheria miezi michache inayokuja.
Mnamo mwezi Novemba mwaka uliopita wabunge walio wengi waliunga mkono pendekezo la kuandaliwa muswada wa sheria ya kuruhusu huduma ya msaada wa kifo kwa kura 330, huku waliopinga wakipata kura 275.
Chini ya mapendekezo ya muswada huo, wagonjwa wenye akili timamu walio na umri kuanzia miaka 18 lakini walio kwenye hali mahututi na wanaokadiriwa kuwa na muda usiozidi miezi sita ya kuishi wataweza kuomba huduma ya kukatisha uhai wao katika miji ya England na Wales. Na ili kutimiza hilo, mgonjwa mahututi atatakiwa kuwa na uwezo wa kumeza mwenyewe dawa zitakazokatisha maisha yake.
Chat Nasi Whatsapp
"Ungana na Wasomaji zaidi ya 12,000 wanaopata huduma ndani ya afyaclass,Kama unachangamoto yoyote ya kiafya;Kwa Ushauri&Tiba tuwasiliane hapa kupitia WhatSapp,Kama huna Whatsapp tuma SMS au Piga +255758286584."
Chat WhatSapp HapaMedical Disclaimer
Medical Disclaimer: Taarifa kwenye makala hii ni kwa ajili ya Updates au elimu ya jumla tu na haichukui nafasi ya uchunguzi,Tiba au ushauri wa kitaalamu wa daktari kwa mtu mmoja mmoja. Kama una dharura au tatizo lolote la kiafya, tafadhali Wasiliana na Daktari moja kwa moja hapa.
Je, unahitaji ushauri binafsi au matibabu ya tatizo lolote?
💬 Wasiliana na Daktari Hapa