Connect with us

Utafiti

Kwanini uwezo wa kupata mimba hupungua baada ya miaka 35?

Avatar photo

Published

on

Kwanini uwezo wa kupata mimba hupungua baada ya miaka 35?

Wanasayansi wanasema, hadi umri wa miaka 35, wanawake wengi hawana matatizo kwenye uzazi, lakini baada ya umri huo uwezekano wa kupata mimba huanza kupungua kwa kasi.

Ni kweli kwamba wanawake wengi wenye umri wa zaidi ya miaka 35 hupata ugumu wa kushika mimba na wakati mwingine wako katika hatari zaidi ya kupata matatizo yanayohusiana na ujauzito na uzazi kuliko wanawake wenye umri wa miaka 20 hadi 35.

Hata hivyo, kupungua kwa uwezo wa kupata mimba ni mchakato wa polepole sana, sio jambo la ghafla, na mchakato huo unatofautiana kutoka kwa mwanamke mmoja hadi mwingine.

“Kuanzia umri wa miaka 35, ubora na wingi wa mayai hupungua kwa kasi,” anasema Lorraine Casavant, daktari wa uzazi na mtafiti katika Chuo cha Imperial London.

Lakini Profesa Anja Bisgaard Pinborg, mkuu wa idara ya uzazi katika kliniki ya Rigshospitalet huko Copenhagen, anasema, “wanawake wengi wana matatizo ya kupata mimba baada ya umri wa miaka 40, hata kama wanakoma hedhi wakiwa na umri wa wastani wa miaka 51.”

Ni vigumu kupata ujauzito

Wataalamu wanaelezea hasa sababu ni mbili; wingi na ubora wa mayai.

Wakati wa kuzaliwa, wanawake huzaliwa na mayai yote ambayo watakuwa nayo. Ni idadi ya mayai karibu milioni mbili, lakini wakifika kubalehe idadi ya mayai ni 600,000 tu.

Na idadi hiyo inazidi kupugua kadiri umri unavyosonga. Umri unaposonga wanawake wanakuwa na mayai machache na ubora wao pia hushuka.

Kwa hivyo inakuwa vigumu zaidi kupata mimba kwa njia ya kawaida na, hata kama utafanya matibabu ya uzazi, kiwango cha mafanikio kwa ujumla kinaweza kuwa chini kuliko ungekuwa mdogo.

Ubora wa yai pia ni muhimu. Umri unaposonga idadi ya mayai yasiyofaa kwa uzazi pia huongezeka.

Hatari ya kuharibika mimba

Uzazi wa wanaume pia huanza kupungua baada ya miaka 30.

“Karibu na umri wa miaka 40, chromosomes 21 hubadilika zaidi, ambayo huongeza hatari ya matatizo ya mimba. Na ndiyo sababu ya mimba nyingi huharibika,” anaeleza Bi. Pinborg.

Utafiti uligundua kwamba hatari ya kuharibika kwa mimba ni karibu asilimia 10% kwa wanawake wenye umri wa miaka 20 hadi 24, lakini hatari huongezeka kwa kasi unapokaribia umri wa miaka 35, ambapo ilizidi asilimia 20%.

Kwa umri wa miaka 42, zaidi ya nusu ya mimba – karibu asilimia 55% – huisha kwa kuharibika. Changamoto za uzazi na mtoto kufa tumboni hutokea zaidi.

Katika utafiti nchini Norway, hatari ya kuzaa mtoto aliyekufa huongezeka kutoka umri wa miaka 35-39 na hatari ni kubwa zaidi katika kundi la umri wa miaka 45-49.

Hata hivyo, hatari ya kuzaliwa mtoto aliyekufa inachangiwa na mambo mengine pia. Mambo kama vile uvutaji sigara, unywaji pombe na unene wa kupindukia huathiri ubora wa yai.

Kwa Wanaume hali Ipoje?

Zaidi ya hayo, kwa kuzingatia sana uzazi wa kike hutufanya tusahau kwamba umri wa mwanaume pia ni muhimu.

Uchunguzi wa wanandoa wa Ulaya ulionyesha kuwa, umri wa mwanaume chini ya miaka 35 hauathiri uwezekano wa kupata mimba, hali hubadilika unapokaribia miaka 40.

“Kati ya wanawake wenye umri wa miaka 35, idadi ya ambao hushindwa kupata mimba huongezeka kwa 18% ikiwa mpenzi wa kiume ana umri wa miaka 35. 28% ikiwa mpenzi wa kiume ana umri wa miaka 40,” utafiti unaonyesha.

Ikiwa mwanaume ni zaidi ya miaka 40, hatari ya kuharibika kwa mimba pia huongezeka. Uchunguzi umeonyesha kuwa ubora wa manii huzorota kadiri umri unavyoongezeka.

Ingawa, ni tofauti na mayai, manii huzaliwa upya kila baada ya miezi miwili hadi mitatu, kupungua kwa ubora kunaweza kutokana na uharibifu wa DNA, sumu ya mazingira na kupungua kwa homoni.

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa4 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa1 month ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa2 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa2 days ago

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi Madhara ya kula nyama ya ng’ombe mbichi Ni desturi ya baadhi ya watu kula...

Magonjwa1 week ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa3 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa4 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...