Connect with us

Magonjwa

Jinsi ya Kupata Mimba haraka,Fahamu hapa Siri hii

Avatar photo

Published

on

Jinsi ya Kupata Mimba haraka,Fahamu hapa Siri hii

Swala la kupata Mimba haraka kwa muda unaotaka wewe,ni changamoto kwa watu wengi, hali ambayo hupelekea migogoro mingi katika mahusiano na hata baadhi ya ndoa kuvunjika.

Zipo Dondoo mbali mbali ambazo ukizizingatia zinaweza kukusaidia kupata Mimba haraka, katika Makala hii tumechambua baadhi ya Njia hizo.

Kupata Mimba haraka

Hizi hapa ni baadhi ya Dondoo za kukusaidia kupata Mimba haraka;

1. Kufanya Mapenzi mara kwa mara;

Fahamu kwamba, uwezekano wa kubeba Mimba huongezeka Zaidi kwa wanandoa au wapenzi ambao hupata muda mwingi wa kufanya mapenzi mara kwa mara,

Tafiti zinaonyesha kwamba; Viwango vya kubeba mimba huongezeka Zaidi kwa Wapenzi wanaofanya mapenzi kila siku au kila baada ya siku moja tofauti na wale ambao hukutana mara chache Zaidi.

2. Kufanya Mapenzi karibu na kipindi cha yai kutoka(ovulation).

Watu wengi huhangaika na swala la kupata Mimba kwa Sababu hufanya mapenzi siku ambazo huwezi kupata Mimba,

Kitu cha kwanza ambacho ni muhimu,unatakiwa kuufahamu vizuri mzunguko wako wa hedhi na kujua “SIKU ZA HATARI” ni Zipi, Maana hapa ndyo unaweza kubeba Mimba.

Ikiwa kujamiiana kila siku haiwezekani – fanya Mapenzi kila baada ya siku 2 hadi 3 kwa wiki kuanzia mara tu baada ya kumalizika kwa kipindi chako cha hedhi. Hii inaweza kusaidia kuhakikisha kwamba unafanya Mapenzi wakati una uwezekano mkubwa wa kubeba Mimba kwa haraka Zaidi.

3. Hakikisha unadhibiti Uzito wako wa Mwili(normal weight).

Watu wengi hawafahamu kwamba, kuwa na Uzito mkubwa(Overweight) au Uzito mdogo Zaidi(underweight) huongeza hatari ya kupata matatizo ya Mayai kutoka kwenye Ovari(ovulation disorders) kwa Mwanamke.

4. Fanya Checkup kwanza kabla ya kuhangaika na Ujauzito,

Wataalam pia wanashauri ufanye Kitu kinaitwa “preconception checkup”.

Kabla ya kuanza kujaribu rasmi, pata uchunguzi kwanza. Muulize daktari wako juu ya vitamini vya ujauzito ambavyo vina folic acid, ambayo husaidia kulinda dhidi ya kasoro kadhaa za kuzaliwa, kama vile spina bifida Foliki asidi hufanya kazi katika hatua za mapema za ujauzito, kwa hiyo ni muhimu kuhakikisha kuwa unapata Foliki asidi ya kutosha kabla na baada ya kupata mimba.

5. Ujue Vizuri Mzunguko wako wa Hedhi

Je! Unajua kiasi gani kuhusu mzunguko wako wa hedhi? Kuelewa kwa kweli hukusaidia kujua wakati unaweza kupata Mimba. Ovulation ndio wakati mzuri zaidi wa kupata mimba. “Huu ndio wakati wa kuzingatia kufanya Mapenzi,”

6. Mkao Sahihi wa kufanya Mapenzi na kupata Mimba,

Usiwe na wasiwasi kuhusu mkao rahisi wa kufanya Mapenzi na kupata Mimba

Kuna dhana nyingi sana kuhusu Mkao mzuri wa kupata mimba, lakini hizo ni dhana tu,

Kwa kweli hakuna ushahidi wa kisayansi unaonyesha kwamba Mkao flani wa kufanya mapenzi kama vile “missionary position” ni bora kuliko mwanamke kuwa juu linapokuja suala la kuongeza nafasi ya kupata mtoto. Na hii inathibitishwa na Majarida mbali mbali ya Wataalam wa afya kama vile WebMd.

Ingawa Mkao wa Kukaa au Kusimama wakati wa kufanya Mapenzi huweza kupunguza kiwango cha mbegu za kiume kupanda juu, kwa Sababu ya gravity inavuta chini.

7. Tulia kidogo kitandani baada ya kufanya Mapenzi

Unashauriwa kutokukimbilia kuamka mara moja baada ya kufanya Mapenzi, tulia kidogo kitandani.

Unashauriwa kutulia kitandani angalau kwa dakika 10 mpaka 15 baada ya kufanya Mapenzi,Usiwahi kwenda bafuni kunawa na maji,

Ikiwa utatulia kwa dakika 10-15, mbegu za kiume(sperm) ambazo zilikuwa zinaenda kwenye Mlango wa kizazi(Cervix) zitakuwa tayari zimeshafika eneo husika.

Hii inaongeza nafasi ya mbegu za kiume kusafiri mpaka kwenye kizazi na kukutana na yai kwa ajili ya Urutubishaji.

8. Hakikisha hufanyi tendo la ndoa ukiwa kwenye hali ya Msongo wa Mawazo(De-stress any way you can).

Jaribu kutofadhaika na kuwa na MSongo wa mawazo sana kuhusu kuanzisha familia. “Tulia tu na itafanyika,”

Fahamu Msongo wa mawazo unaweza kutatiza hata yai kutoka kwenye Ovari(ovulation) na kupunguza Zaidi uwezo wa wewe kubeba mimba kwa wakati unaohitaji.

9. Pamoja na Dondoo Zingine za kubadilisha mtindo wa Maisha zinaweza kukusaidia kupata Mimba kwa haraka,Mfano;

  • Kuacha kabsa Matumizi ya Pombe kwa mwanamke na Mwanaume
  • Kuacha kabsa Uvutaji wa Sigara au kutumia kilevyi cha aina yoyote
  • Kutokutumia dawa pasipo maelekezo kutoka kwa Wataalam wa afya n.k

Ni matumaini Yangu umejifunza Dondoo muhimu za Kukusaidia kubeba Mimba kwa haraka Zaidi…!!!!

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In https://afyaclass.com Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 months ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa3 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa3 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa5 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake5 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa4 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa2 days ago

kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani

kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani Unapopata tatizo la kuharisha na kutapika kwa wakati mmoja unaweza kuwaza sana,...

Magonjwa4 days ago

Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu

Dalili za infection kwenye damu Mchafuko wa damu,chanzo,dalili na Tiba Mchafuko wa damu; hiki ni kiswahili ambacho watu wamezoea kukitumia...

Magonjwa7 days ago

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri Yapo magonjwa mbali mbali ya ngozi ambayo huweza kuathiri Sehemu za Siri za Mwanaume...

Magonjwa2 weeks ago

Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu

Dalili za acid reflux: Tatizo la Gastroesophageal reflux disease (GERD), ni tatizo ambalo huwapata Watu wengi,Tatizo hili hujulikana kwa jina...

Magonjwa4 weeks ago

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe au ni ugonjwa ambao huhusisha ngozi kupoteza rangi...

Magonjwa4 weeks ago

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni,...

Magonjwa1 month ago

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu Utangulizi: Scabies huhusisha mtu kuwa na vipele na muwasho kwenye ngozi yake ambapo...

Magonjwa1 month ago

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume Gono ni neno maarufu ambalo kirefu chake ni Gonorrhea na kiswahili chake ni...

Magonjwa1 month ago

Dalili Mpya za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni Dalili za ukimwi kwenye ngozi Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala...

Magonjwa1 month ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Trending