Connect with us

Jukwaa la Midahalo(Discussions Corner)

WHO yaonya maambukizi mapya ya HIV na Vifo kuongezeka baada ya ARVs kusitishwa

Published

on

WHO yaonya maambukizi mapya ya HIV na Vifo kuongezeka baada ya ARVs kusitishwa

Shirika la Afya Duniani (WHO) limeonya maambukizi mapya ya HIV zaidi ya milioni 10 na vifo vya Watu milioni 3 vinavyohusiana na UKIMWI vinaweza kushuhudiwa kufuatia kusitishwa kwa msaada wa kigeni wa Marekani unaosaidia upatikanaji wa dawa za kufubaza makali ya virusi vya UKIMWI, ARVs.

Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Tedros Adhanom Ghebreyesus WHO amesema hatua ya Marekani kujiondoa kusaidia mapambano ya HIV imeathiri usambazaji wa dawa katika nchi saba za Afrika, zikiwemo Kenya, Lesotho, Sudan Kusini, Burkina Faso, Mali, Nigeria, na Haiti, ambazo zinaweza kuishiwa dawa ndani ya miezi michache ijayo. 

Dr. Tedros amesema kusitishwa kwa msaada huo wa Marekani kunaweza kufuta mafanikio ya miaka 20 katika kupambana na HIV huku pia akionya kuwa juhudi za kudhibiti magonjwa mengine kama polio, malaria, na kifua kikuu zimeathirika vibaya na ameiomba Marekani kuhakikisha kuwa inatoa muda wa mpito kwa nchi zilizoathirika ili ziweze kupata vyanzo mbadala vya fedha badala ya kusitisha msaada kwa ghafla, hatua ambayo inaweza kusababisha madhara makubwa ya kiafya duniani. 

Itakumbukwa Rais wa Marekani, Donald Trump alitangaza mwezi huu kusitisha kutoa fedha za misaada kupitia miradi iliyokuwa chini ya Shirika lake la misaada la USAID, hali iliyoibua taharuki hasa kwa nchi nyingi za Afrika zinazotegemea fedha za ufadhili kushughulika na magonjwa kama Ukimwi.

KARIBU DISCUSSION CORNER,WEKA COMMENT YAKO HAPA CHINI JUU YA MADA HII

#Afya News

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

500

Atumia siku 1,500 kukuza nywele ili kumsaidia mchumba wake wenye alopecia

Published

on

Atumia siku 1,500 kukuza nywele ili kumsaidia mchumba wake wenye alopecia

Mwanamume huyu alitumia karibu siku 1,500 kukuza nywele zake akiwa na lengo moja mahususi akilini: kumpa mchumba wake wigi la asili linalobeba sehemu yake. Uamumizi huo ni kumsaidia mchumba wake mwenye tatizo la nywele kutokuota kichwani au alopecia.

Hapo Vipi? Wanaume😂😂

#love #relationshipgoals #alopecia

Continue Reading

Jukwaa la Midahalo(Discussions Corner)

Breaking: Chukueni tahadhari dhidi ya uwepo wa COVID 19

Published

on

Breaking: Chukueni tahadhari dhidi ya uwepo wa COVID 19

Wizara ya Afya imesema imeendelea kufanya ufuatiliaji wa karibu na kutoa taarifa za kila siku kuhusu magonjwa ya mlipuko pamoja na tetesi za uwepo wa magonjwa hayo nchini ambapo imesema tangu February hadi April 2025, ufuatiliaji wa virusi vya Covid 19 umeonesha ongezeko la maambukizi kutoka 1.4% (Wagonjwa wawili kati ya Watu 139 waliopimwa) mwezi February hadi 16.3% (Wagonjwa 31 kati ya 190 waliopimwa) mwezi March, na kisha 16.8% (Wagonjwa 31 kati ya Watu 185 waliopimwa) mwezi Aprili 2025.

Taarifa iliyotolewa leo May 20,2025 na Mganga Mkuu wa Serikali, Dkt. Grace Magembe imesema “Ugonjwa wa UVIKO-19, ambao ulitangazwa kwa mara ya kwanza nchini March 2020, umeendelea kuwepo kwa kiwango cha chini kama yalivyo magonjwa mengine ya mfumo wa njia ya hewa, hali ya kuongezeka na kupungua kwa ugonjwa huu imekuwepo kila mwaka tangu kutangazwa kwa ugonjwa huu mwaka 2020, kwa kipindi hiki ongezeko hili linaonekana zaidi katika Mkoa wa Dar es salaam, Wizara ya Afya inaendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa magonjwa ya mfumo wa njia ya hewa nchini na kutoa taarifa”

“Katika kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Aprili 2025, tumeshuhudia ongezeko la tetesi zinazohusiana na magonjwa ya mfumo wa njia ya hewa katika jamii hapa nchini, hasa katika mkoa wa Dar es salaam, kwa kutumia mifumo ya ufuatiliaji wa magonjwa ya mfumo wa njia ya hewa, ambayo imekuwepo tangu mwaka 2008, tumekuwa tukifuatilia mwenendo wa magonjwa haya ili kubaini aina za vimelea vinavyosababisha maambukizi, ongezeko la visa, pamoja na uwezekano wa kujitokeza kwa kirusi kipya chenye uwezo wa kusambaa kwa haraka”

“Vipimo vya maabara vimebaini kuongezeka na kupungua kwa virusi vya influenza hali ambayo imekuwa ikionekana pia katika miaka iliyopita na ndiyo maana hujulikana kama ‘Seasonal influenza”, vipimo vimeonesha kuwa hakuna kirusi kipya kinachoweza kusambaa kwa haraka na kusababisha mlipuko wa aina ya Pandemiki” Cc:MillardAyoUPDATES

Continue Reading

Jukwaa la Midahalo(Discussions Corner)

Nimefanyiwa upasuaji mara 100 na siachi’ Nini Ushauri wako hapa

Published

on

Nimefanyiwa upasuaji mara 100 na siachi’ Nini Ushauri wako hapa

Abby Wu alikuwa na umri wa miaka 14 tu alipofanyiwa upasuaji wa urembo bandia kwa mara ya kwanza.

Baada ya kupata matibabu ya homoni, uzito wa mwili wa Abby uliongezeka kutoka kilo 42 hadi kilo 62 ndani ya miezi miwili.

Mwalimu wake wa michezo ya kuigiza aligundua mabadiliko hayo ya mwili.

Mwalimu wangu aliniambia, ”ulikuwa nyota lakini sasa umekuwa mnene kupita kiasi. Chagua moja uondoke kwa tasnia hii au upunguze kilo,” anakumbuka alichoambiwa kipindi hicho akisubiri kufanya mtihani wake wa tamthilia.

Mama yake Abby aliingilia kati na kuamua kumpeleka kufanyiwa upasuaji wa kuondoa mafuta tumboni na miguuni.

Abby anavuta kumbukumbu jinsi mamake alivyompa motisha akisubiri kufanyiwa operesheni hiyo.

”Kuwa mkakamavu na uingie ufanyiwe. Ukitoka hapo utakuwa mrembo zaidi.”

Upasuaji huo ulimuacha na makovu. Abby alipatiwa dawa za kupunguza uchungu lakini alikuwa macho akifanyiwa operesheni hiyo.

”Ningeona kiasi cha mafuta kilichotolewa mwilini mwangu na damu iliyokuwa ikinivuja,” anasema.

“Upasuaji ulifanya kazi. Nilijiamini na kuwa na furaha zaidi, siku baada ya siku. Nadhani mama yangu alifanya chaguo sahihi.”

Sasa Abby ana umri wa miaka 35 na amefanyiwa upasuaji wa urembo mara mia moja ikimgharimu dola nusu milioni.

Anamiliki kliniki ya ulimbwende katikati mwa mji wa Beijing na amekuwa mtu tajika katika tasnia ya upasuaji wa plastiki nchini China.

Lakini upasuaji huo pia unaathari zake kwa mwili.

Akiwa amekaa mbele ya kioo anajipodoa ili kuficha makovu ya sindano za kupunguza unene usoni, utaratibu anaoufanya kila mwezi ili kuhakikisha uchanga usoni mwake nakuhakikisha hana ngozi zilizolegea baada ya upasuaji wa kupunguza taya uliondoa mifupa mingi.

Lakini anasisitiza kuwa hajutii upasuaji wa urembo aliyofanya kufikia sasa akiamini kuwa mamake hakukosea kumuanzisha katika ulimbwende huu.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2017 Zox News Theme. Theme by MVP Themes, powered by WordPress.