Connect with us

Magonjwa

Tatizo la kupoteza Usikivu: Sababu, Dalili, na Matibabu

Avatar photo

Published

on

Tatizo la kupoteza Usikivu: Sababu, Dalili, na Matibabu

Kwa Mujibu wa Shirika la afya Duniani(WHO)

Kufikia 2050 karibu watu bilioni 2.5 wanakadiriwa kuwa na kiwango fulani cha upotevu wa Usikivu na angalau milioni 700 watahitaji urekebishaji wa kusikia yaani hearing rehabilitation.

Tatizo la kupoteza usikivu linaweza kuwa kizingiti kikubwa kwa maisha ya kila siku. Kwa bahati mbaya, tatizo hili la kiafya linaweza kuwaathiri watu wote, wakiwemo watoto, watu wazima, na wazee. Kwa hivyo, ni muhimu kufahamu sababu za tatizo la usikivu, dalili zake, na matibabu yanayopatikana.

YALIYOMO:

  1. Sababu za Tatizo la kupoteza Usikivu
  2. Aina za Tatizo la kupoteza Usikivu
  3. Dalili za Tatizo la kupoteza Usikivu
  4. Jinsi ya Kutambua Tatizo la kupoteza Usikivu
  5. Matibabu ya Tatizo la kupoteza Usikivu
  6. Njia za Kuzuia Tatizo la kupoteza Usikivu
  7. Maswali Yanayoulizwa Mara kwa Mara kuhusu Tatizo la kupoteza Usikivu
  8. Hitimisho

Sababu za Tatizo la kupoteza Usikivu

Tatizo la kupoteza usikivu linaweza kuchangiwa na sababu nyingi, ikiwa ni pamoja na:

(1) Mtoto

– Swala la kigenetic,uwepo wa genes au vinasaba vya tatizo

– Maambukizi kwa mtoto akiwa bado tumboni yaani intrauterine infections – kama vile ya rubella pamoja na cytomegalovirus infection.

– Mtoto kuzaliwa akiwa na tatizo la kukosa hewa ya oxygen yaani birth asphyxia

– Mtoto kupata tatizo la manjano wakati wa kuzaliwa yaani hyperbilirubinemia (severe jaundice in the neonatal period)

– Mtoto kuzaliwa na tatizo la Uzito mdogo sana(low-birth weight) n.k

(2) Sababu kwa Ujumla

• Kupata maambukizi ya Sikio au masikio kwa muda mrefu

• Kupatwa na tatizo la meningitis pamoja na maambukizi mengine

• Tatizo la Maji kukusanyika kwenye eneo la ndani ya Sikio

• Kuweka maji kwenye sikio mfano wakati wa kuoga au kujisafisha n.k

• Uvutaji wa Sigara,Pia huongeza hatari ya kupata tatizo la kupoteza usikivu

• Kupata ajali au kuumia eneo la masikio pamoja na kichwani

• Kuwa kwenye sehemu zenye makelele sana mara kwa mara

• Tatizo la otosclerosis

• Kuwa na uchafu zaidi ambao umeganda ndani ya sikio au kuziba sikio/masikio

• Upotevu wa usikivu wa gafla kutokana na uharibu wa nerves yaani sudden sensorineural hearing loss.

• Kutumia dawa zinazoweza kuharibu masikio, ototoxic medicines

• Upungufu wa baadhi ya virutubisho muhimu

• Umri kuwa mkubwa zaidi au Kuzeeka

• Kupata mshtuko wa sauti kali n.k

Aina za Tatizo la Kupoteza Usikivu

Kuna aina mbili za tatizo la kupoteza usikivu:

  • Tatizo la kupoteza usikivu la kudumu: hili ni tatizo la kudumu ambalo linahitaji matibabu ya kina ili kupunguza athari zake kwa maisha ya kila siku.
  • Tatizo la kupoteza usikivu la muda mfupi: hili ni tatizo la muda mfupi ambalo linaweza kuisha bila hata matibabu yoyote.

Dalili za Tatizo la kupoteza Usikivu

Dalili za tatizo la kupoteza usikivu ni pamoja na:

– Mtu Kushindwa kusikia sauti za chini au sauti za juu

– Mtu Kushindwa kusikia wakati wa mazungumzo

– Mtu Kushindwa kusikia sauti za TV au redio

– Kupata maumivu au kutokwa na damu kwenye sikio

– Kutokwa na maji kwenye sikio

– Kupata mshtuko wa sauti kali

– Kusikia kelele isiyo ya kawaida ndani ya masikio yako n.k

Jinsi ya Kutambua Tatizo la kupoteza Usikivu

Kwa kawaida, kama unashindwa kusikia vizuri, au inakuwa vigumu kusikia sauti ya watu wanaokuzunguka, unapaswa kutafuta ushauri wa daktari wa masikio. Madaktari hawa watafanya vipimo ili kujua kwa nini unashindwa kusikia vizuri.

Vipimo hivi ni pamoja na:

  • Vipimo vya sikio: Daktari atatumia kifaa maalum cha kujaribu kusikia sauti yako kwenye sikio. Kwa kutumia vipimo hivi, daktari ataweza kujua kama una tatizo la kupoteza usikivu na sababu za tatizo hilo.
  • Vipimo vya uwezo wa kusikia: Daktari atafanya vipimo ili kujua uwezo wako wa kusikia sauti za aina tofauti.
  • Vipimo vya ubongo: Vipimo hivi vinaweza kufanyika ili kujua ikiwa tatizo la kupoteza usikivu limeathiri ubongo wako.

Matibabu ya Tatizo la kupoteza usikivu Usikivu

Matibabu ya tatizo la kupoteza usikivu yanategemea sababu za tatizo hilo,

Ikiwa tatizo la kupoteza usikivu limechangiwa na maambukizi ya sikio, daktari atakupa dawa za kupunguza maumivu na kuzuia maambukizi kuendelea.

Ikiwa tatizo la kupoteza usikivu limechangiwa na uharibifu wa sikio, daktari atakupa chaguzi za matibabu kama vile vifaa vya kusaidia kusikia, matibabu ya upasuaji au vifaa vya kusaidia sikio n.k.

Njia za Kuzuia Tatizo la kupoteza Usikivu

Kuna njia kadhaa ambazo unaweza kutumia ili kuzuia tatizo la kupoteza usikivu, kama vile:

✓ Kuvaa vifaa vya kinga kwenye masikio yako wakati wa shughuli zinazohusisha makele mengi au wakati wa muziki mkubwa.

✓ Kuepuka kutumia vifaa vya sauti kwa muda mrefu sana ikiwa ni pamoja na kuvaa earphone kwa muda mrefu huku ukisikiliza mziki kwa sauti kubwa.

✓ Kuepuka kuweka maji kwenye sikio lako hasa wakati wa kujisafisha au kuoga,jisafishe kwa uangalifu huku ukiepuka kuweka maji ndani ya sikio lako

✓ Kufanya usafi sahihi wa masikio yako ili kuzuia maambukizi.

FAQs:Maswali Yanayoulizwa Mara kwa Mara kuhusu Tatizo la kupoteza Usikivu

[sc_fs_multi_faq headline-0=”h3″ question-0=”Ni vipi tatizo la kupoteza usikivu linaweza kutibiwa?” answer-0=”Matibabu ya tatizo la kupoteza usikivu yanategemea sababu za tatizo hilo. Ikiwa tatizo la usikivu limechangiwa na maambukizi ya sikio, daktari atakupa dawa za kupunguza maumivu na kuzuia maambukizi kuendelea. Ikiwa tatizo la usikivu limechangiwa na uharibifu wa sikio, daktari atakupa chaguzi za matibabu kama vile vifaa vya kusaidia kusikia, matibabu ya upasuaji au vifaa vya kusaidia sikio n.k.” image-0=”” headline-1=”h3″ question-1=”Je, kuna njia yoyote ya kuzuia tatizo la kupoteza usikivu?” answer-1=”Njia kadhaa za kuzuia tatizo la kupoteza usikivu ni pamoja na kuvaa vifaa vya kinga kwenye masikio wakati wa shughuli zinazohusisha makelele zaidi au wakati wa muziki mkubwa, kuepuka kutumia vifaa vya sauti kwa muda mrefu sana, kuepuka kuweka maji kwenye sikio lako, na kufanya usafi sahihi wa masikio yako ili kuzuia maambukizi.” image-1=”” count=”2″ html=”true” css_class=””]

Hitimisho

Tatizo la kupoteza usikivu ni tatizo linaloweza kuathiri watu wa umri wowote. Ikiwa una shida ya kusikia, ni muhimu kutafuta ushauri wa daktari wa masikio ili kujua sababu za tatizo hilo na kupata matibabu sahihi,

Kuna njia kadhaa za kuzuia tatizo la kupoteza usikivu, kama vile kuvaa vifaa vya kinga kwenye masikio, kuepuka kutumia vifaa vya sauti kwa muda mrefu sana, na kufanya usafi sahihi wa masikio yako.

Kumbuka, kinga ni bora kuliko tiba, na kuzuia tatizo la kupoteza usikivu kunaweza kusaidia kulinda afya yako ya masikio kwa muda mrefu.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In https://afyaclass.com Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 months ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa3 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa3 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa5 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake5 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa4 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa2 days ago

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri Yapo magonjwa mbali mbali ya ngozi ambayo huweza kuathiri Sehemu za Siri za Mwanaume...

Magonjwa6 days ago

Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu

Dalili za acid reflux: Tatizo la Gastroesophageal reflux disease (GERD), ni tatizo ambalo huwapata Watu wengi,Tatizo hili hujulikana kwa jina...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe au ni ugonjwa ambao huhusisha ngozi kupoteza rangi...

Magonjwa3 weeks ago

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni,...

Magonjwa4 weeks ago

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu Utangulizi: Scabies huhusisha mtu kuwa na vipele na muwasho kwenye ngozi yake ambapo...

Magonjwa4 weeks ago

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume Gono ni neno maarufu ambalo kirefu chake ni Gonorrhea na kiswahili chake ni...

Magonjwa1 month ago

Dalili Mpya za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni Dalili za ukimwi kwenye ngozi Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala...

Magonjwa1 month ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Magonjwa1 month ago

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake Karibu! Hapa kwa makala yenye taarifa muhimu kuhusu...

Magonjwa1 month ago

Vyanzo Vya Kifo cha Ghafla: Sababu Zinazotisha na Jinsi ya Kujikinga

“Vyanzo Vya Kifo cha Ghafla: Sababu Zinazotisha na Jinsi ya Kujikinga” Kifo cha ghafla ni janga lisilotarajiwa ambalo linaweza kumpata...

Trending