Connect with us

afyatips

Dalili za blood infection,Maambukizi kwenye Damu

Doctor Ombeni

Published

on

111 Views
0 Comments

Dalili za blood infection,Maambukizi kwenye Damu

Blood Infection hapa tunazungumzia maambukizi ya vimelea mbali mbali vya Magonjwa kwenye damu, Vimelea hivo huweza kuwa Bacteria, Fangasi, Virusi n.k.

Maambukizi haya wakati mwingine huweza kufikia hatua ya kuitwa Sepsis.

Sepsis ni pale ambapo mwili wako unakuwa na mwitikio mkali dhidi ya maambukizi kwenye damu. Wakati huo mfumo wako wa kinga, ambao kwa kawaida unakukinga dhidi ya vijidudu, huanza kushambulia tishu za mwili wako.

Maambukizi ya damu, yanayojulikana kitaalamu kama sepsis, ni hali hatari inayotokea wakati mwili unajibu maambukizi kwa njia isiyo ya kawaida, kisha kusababisha kuvimba mwili mzima, kushindwa kwa viungo, au hata kifo. Sepsis inaweza kusababishwa na bakteria, virusi, fangasi, au vimelea vinavyosambaa kupitia damu na kuathiri viungo muhimu kama moyo, mapafu, figo, na ubongo.

Chanzo cha Maambukizi ya Damu

Maambukizi haya mara nyingi hutokana na:

Maambukizi ya bakteria – Kama vile Staphylococcus aureus, Escherichia coli (E. coli), na Streptococcus pneumoniae.n.k

Maambukizi ya virusi – Kama virusi vya dengue, HIV, na hepatitis.

Maambukizi ya fangasi – Kama Candida kwa watu wenye kinga dhaifu.

Maambukizi kutoka kwenye vidonda – Vidonda vikubwa au vidogo vinaweza kuwa mlango wa bakteria kuingia kwenye damu.

Maambukizi ya mfumo wa mkojo, mapafu, tumbo, au ngozi – Maambukizi kwenye damu mara nyingi huanza kutokana na maambukizi haya.

Matumizi ya vifaa vya matibabu – Katheta za mkojo, (IV lines), au mashine za kupumua zinaweza kusababisha maambukizi endapo hazitatunzwa vizuri kwenye hali ya Usafi wa hali ya juu.

Dalili za Maambukizi ya Damu

Dalili za maambukizi kwenye damu zinaweza kutofautiana, lakini kwa Ujumla huweza Kujumuisha:

1. Homa kali (joto la mwili kupanda au kushuka sana)

2. Mapigo ya moyo kuwa ya haraka (tachycardia)

3. Kupumua kwa shida au haraka

4. Mwili kutetemeka sana

5. Kuwa dalili kama za Kuchanganyikiwa au kupoteza fahamu

6. Kupata upele kwenye ngozi(Skin rashes)

7. Maumivu makali mwilini

8. Kukojoa kidogo sana kuliko kawaida au kutokukojoa kabsa.

9. Kuhisi kichefuchefu na kutapika

10. Kupata tatizo la Kuharisha

11. Mwili kuchoka sana, kuwa dhaifu au kukosa nguvu

12. Kutoa sana jasho

13. Kupata maumivu makali ikiwemo ya kichwa n.k

14. Kuhisi kizunguzungu

15. Kuhisi usingizi sana

16. Ngozi kuwasha sana n.k

Ukipata Dalili kama hizi,hakikisha Unapata Msaada mapema!

Tiba au Matibabu ya Maambukizi ya Damu

Matibabu ya maambukizi kwenye damu yanahitaji hatua za haraka ili kuokoa maisha hasa ikiwa ni Sepsis. Njia kuu za matibabu ni hutegemea na chanzo husika,Mfano; Matumizi ya Antibiotiki -kama chanzo ni maambukizi ya bakteria.n.k.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

111 Views
0 Comments

Medical Disclaimer

Medical Disclaimer: Taarifa kwenye makala hii ni kwa ajili ya Updates au elimu ya jumla tu na haichukui nafasi ya uchunguzi,Tiba au ushauri wa kitaalamu wa daktari kwa mtu mmoja mmoja. Kama una dharura au tatizo lolote la kiafya, tafadhali Wasiliana na Daktari moja kwa moja hapa.

Je, unahitaji ushauri binafsi au matibabu ya tatizo lolote?

💬 Wasiliana na Daktari Hapa

🏆Certified| Doctor from Afyaclass. Maudhui haya ni kwa ajili ya elimu ya jumla ya afya. Unapohitaji ushauri wa kina, uchunguzi, au matibabu binafsi, wasiliana na daktari kupitia namba:+255758286584.Pia tufwatilie kupitia: @Facebook | @Instagram | @YouTube.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Guest Avatar

LATEST POSTS

magonjwa ya wanawake5 years ago

PID NI NINI? Na Dalili zake ni Zipi?(magonjwa ya Wanawake)

 PID • • • • • PID NI NINI? Na Dalili zake ni Zipi?(magonjwa ya Wanawake) PID NI NINI?  PID...

afyatips19 hours ago

Dalili za kidonda cha operation kupona

DALILI ZA KIDONDA CHA OPERATION KUPONA Baada ya kufanyiwa operation, mwili huanza mchakato wa kuponya kidonda mara moja. Mchakato huu...

Utafiti22 hours ago

Desogestrel yahusishwa na Kuongezeka kwa Hatari ya uvimbe wa ubongo

Mamlaka ya Dawa na Bidhaa za Afya ya Ufaransa (ANSM) imewaonya wanawake wanaotumia baadhi ya njia za uzazi wa mpango...

magonjwa5 years ago

UGONJWA WA BRUCELLA(chanzo,dalili na tiba)

UGONJWA WA BRUCELLA(chanzo,dalili na tiba) Huu ni ugonjwa ambao kwa kitaalam hujulikana kama brucellosis na chanzo chake ni bacteria wanaojulikana...

magonjwa ya watoto2 years ago

Ugonjwa wa Surua kwa Watoto: Sababu, Dalili, Matibabu na Kinga

Ugonjwa wa Surua kwa Watoto: Sababu, Dalili, Matibabu na Kinga Ugonjwa wa Surua ni ugonjwa wa kuambukiza sana kwa watoto...

Afya News2 days ago

Vifo vya Watoto Wachanga Katika Mlipuko wa Surua Pennsylvania na Mjadala wa Afya ya Umma

Mlipuko wa ugonjwa wa surua (measles) unaoendelea katika jimbo la Pennsylvania, Marekani, umeendelea kuzua wasiwasi mkubwa baada ya watoto wawili...

Afya News2 days ago

Wauguzi Kenya Wasitisha Mgomo Baada ya Makubaliano na Serikali

Wauguzi nchini Kenya wamesitisha mgomo wao wa siku 43 baada ya kufikia makubaliano na serikali kupitia chama chao cha wafanyakazi....

WHO3 days ago

Uvutaji Sigara Unaongeza Uwezekano wa Ugumba

Uvutaji Sigara Unaongeza Uwezekano wa Ugumba Shirika la Afya Duniani (WHO) limeonya kuwa matumizi ya tumbaku yana athari kubwa kwa...

magonjwa ya wanaume1 year ago

Dalili za Gono Sugu kwa Mwanaume (Gonorrhea sugu)

Gono sugu ni maambukizi ya zinaa yanayosababishwa na bakteria aitwaye Neisseria gonorrhoeae, ambayo yamekuwa yakujirudia rudia na hayaponi kwa baadhi...

Uzazi/Ujauzito4 days ago

Madhara ya Sindano ya depo,Fahamu hapa

Madhara ya Sindano ya Depo (Depot Medroxyprogesterone Acetate – DMPA) Sindano ya Depo-Provera (Depot Medroxyprogesterone Acetate – DMPA) ni mojawapo...

112
0