News
Changamoto ya umasikini inachangia kwa kiasi kikubwa maambukizi ya VVU na Ukatili wa kijinsia
Changamoto ya umasikini inachangia kwa kiasi kikubwa maambukizi ya VVU na Ukatili wa kijinsia
Dodoma, Tanzania
Januari 27, 2023 Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Zainab Chaula alikutana na kufanya mazungumzo na Rais na Mtendaji Mkuu wa shirika la “Elizabeth Glaser Pediatric Aids Foundation (EGPAF)” Bw. Chip Lyons ambapo wamejadili ushirikiano wa kutokomeza maambukizi ya VVU kwa Wanawake na watoto jijini Dodoma.
Dkt. Chaula amesisitiza kuwawezesha wananchi kiuchumi hususani Wanawake ili kukabiliana na changamoto ya umasikini ambao unachangia kwa kiasi kikubwa maambukizi ya VVU na Ukatili wa kijinsia.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jinsia Badru Abdulnuru, Mkurugenzi wa EGPAF Tanzania Dkt. Sajida Kimambo, Mkurugenzi wa ufundi wa EGPAF Dkt. Roland Ven pamoja na wataalamu wengine wa shirika la EGPAF na Wizara wamehudhuria kikao hicho kilichofanyika kwenye Ofisi za Wizara Jijini Dodoma.
#@maendeleoyajamii
-
Uzazi/Ujauzito6 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Uzazi/Ujauzito4 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa5 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Magonjwa3 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events7 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News5 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
afyatips19 hours ago
Madhara ya damu kuwa nyingi mwilini
-
Utafiti2 days ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO