Connect with us

Magonjwa

Madhara ya Kunywa Maji Mengi: Hatari ya Kuzidisha Kiasi cha Maji Kwenye Mwili Wako

Avatar photo

Published

on

Madhara ya Kunywa Maji Mengi: Hatari ya Kuzidisha Kiasi cha Maji Kwenye Mwili Wako

Kunywa maji mengi ni muhimu sana kwa afya ya mwili wako. Maji husaidia kudumisha kiwango sahihi cha unyevu kwenye mwili wako, na pia husaidia katika utendaji mzuri wa seli zote kwenye mwili wako.

Lakini, kama ilivyo kwa mambo mengine yote, ukifanya kupita kiasi inaweza kusababisha madhara. Katika makala hii, tutajadili madhara ya kunywa maji mengi na jinsi ya kuzuia madhara haya.

Ingawa ni mara chache sana huleta madhara,Unapokunywa maji mengi kupita kiasi unaweza kupata tatizo linalojulikana kama water poisoning, intoxication, or kuathiri utendaji kazi wa ubongo wako. Hii hutokea wakati kuna maji mengi katika seli (ikiwa ni pamoja na seli za ubongo), na kuzifanya seli hizi kuvimba.

Tunafahamu kwamba,Seli zote za mwili zinahitaji Maji ili kufanya kazi vizuri, Shida hutokea pale ambapo umekunywa maji mengi kupita kiasi na kusababisha tatizo ambalo kwa kitaalam hujulikana kama overhydration.

Ingawa hakuna Kanuni au formula moja ya kutumia ili kujua unatakiwa kunywa maji kiasi gani kila siku,

Wataalam wengi wanashauri kunywa Maji angalau glass Nane(8) za Maji kwa siku, au kunywa Lita 2.5 mpaka 3 za Maji kwa Siku,

Hata hivo kiasi hiki cha kunywa Maji kila Siku huweza kuathiriwa na hali ya mazingira kama vile;

  • baridi,
  • Joto,
  • Jua,
  • Mvua,
  • Ufanyaji wa Mazoezi,
  • afya yako ya mwili kwa ujumla,
  • na hali zingine kama vile kuwa Mjauzito au kunyonyesha.

NINI HUTOKEA ENDAPO UMEKUNYWA MAJI KUPITA KIASI?

Unapokunywa maji mengi kupita kiasi unaweza kupata tatizo linalojulikana kama water poisoning, intoxication, au kuathiri utendaji kazi wa ubongo wako.

Hii hutokea wakati kuna maji mengi katika seli (ikiwa ni pamoja na seli za ubongo), na kuzifanya seli hizi kuvimba,

Wakati seli hizi kwenye Ubongo zikivimba huweza kusababisha hali ya mgandamisho(Pressure) ndani ya Ubongo wako, na hapa ndyo utaanza kuona dalili kama vile;

  • Maumivu ya kichwa,
  • kupata kizunguzungu,
  • kuhisi kuchaganyikiwa(confusion),
  • hali ya kusinzia(drowsiness),
  • kupoteza fahamu
  • Na hata wakati mwngine kupoteza maisha n.k

Na kama huu mgandamizo ukiongezeka zaidi huweza kupelekea tatizo la Shinikizo la damu-hypertension (High Blood Pressure),Tatizo la mapigo ya moyo kushuka- bradycardia (Low Heart Rate) n.k.

Lakini pia Sodium ni mojawapo ya electrolyte ambayo huathiriwa zaidi na kunywa maji mengi kupiga kiasi na kupelekea tatizo la hyponatremia.

Madhara ya Kunywa Maji Mengi

Kunywa maji mengi kuliko mwili wako unavyohitaji kunaweza kuwa na madhara makubwa, Baadhi ya madhara haya ni pamoja na:

1. Kuathiri kiwango cha SODIUM,

Sodium ni mojawapo ya electrolyte ambayo huathiriwa zaidi na kunywa maji mengi kupiga kiasi na kupelekea tatizo la hyponatremia,

Na tatizo hili huweza kupelekea matatizo mengine kama vile;

  • kusababisha kichefuchefu,
  • Mtu kutapika,
  • Kupata kizunguzungu,
  • au hata kuzirai.

2. Kusababisha ugonjwa wa moyo,

Kunywa maji mengi kupita kiasi kunaweza kusababisha tatizo la moyo kushindwa kufanya kazi(heart failure),

Kwa sababu ya Maji kuwa mengi, moyo wako unaweza kushindwa kusukuma damu kwa ufanisi. Hii inaweza kusababisha tatizo la shinikizo la damu, kiharusi, au hata kufa kwa ghafla.

3. Kusababisha kuharisha na kichefuchefu,

Kunywa maji mengi kunaweza kusababisha kuharisha na kichefuchefu,

Hii ni kwa sababu maji mengi yanaweza kusababisha tumbo lako kujaa na kusababisha shida kwenye umeng’enyaji wa chakula.

4. Kusababisha uvimbe kwenye ubongo

Kunywa maji mengi kupita kiasi kunaweza kusababisha uvimbe kwenye ubongo,

Hii ni kwa sababu kunywa maji mengi kupita kiasi kunaweza kusababisha kuvuja kwa maji kwenye tishu za ubongo wako, na kusababisha uvimbe kwenye seli za Ubongo.

Jinsi ya Kuzuia Madhara ya Kunywa Maji Mengi

Ili Kuzuia madhara ya kunywa maji mengi, Unapaswa kuzingatia vidokezo hivi:

✓ Kunywa maji kwa kiwango kinachohitajika

Unapaswa kunywa maji kwa kiwango kinachohitajika na sio kupita kiasi.

Kila mtu ana kiwango chake cha maji kinachohitajika kwa siku, ambacho kinategemea na umri, uzito, na shughuli za kila siku.

Unaweza kujua kiwango chako cha maji kinachohitajika kwa siku kwa kuzungumza na daktari wako.

✓ Kunywa maji kwa vipindi virefu

Badala ya kunywa maji yote kwa wakati mmoja, unapaswa kunywa maji kidogo kidogo kwa vipindi virefu.

Hii inasaidia mwili wako kumeng’enya maji vizuri na kuzuia matatizo kama vile kuharisha na kichefuchefu.

✓ Epuka kunywa maji kabla ya kula

Kunywa maji mengi kabla ya kula kunaweza kusababisha kupungua kwa asidi ya tumboni, ambayo inaweza kusababisha shida za kumeng’enya chakula baada ya kula. Unapaswa kunywa maji kwa saa moja au mbili baada ya kula.

✓ Punguza kunywa vinywaji vyenye sukari nyingi

Kunywa vinywaji vyenye sukari nyingi kama soda na juisi za dukani kwa kiwango kikubwa kunaweza kusababisha kushuka kwa usawa wa chumvi au Electrolyte kama Sodium kwenye mwili wako.

Kwa hiyo, unapaswa kuzingatia kupunguza kiasi cha vinywaji hivi na badala yake kunywa maji Zaidi.

FAQs:Maswali Yanayoulizwa Sana

[sc_fs_multi_faq headline-0=”h3″ question-0=”Je, kunywa maji mengi kunaweza kusababisha madhara?” answer-0=”Ndio, kunywa maji mengi kupita kiasi kunaweza kusababisha madhara kama vile kuathiri kiwango cha Sodium mwilini, kusababisha ugonjwa wa moyo, kusababisha kuharisha na kichefuchefu, na hata kusababisha uvimbe kwenye ubongo.” image-0=”” headline-1=”h3″ question-1=”Je, ni kiasi gani cha maji kinachohitajika kwa siku?” answer-1=”Kiwango cha maji kinachohitajika kwa siku kinategemea umri, uzito, na shughuli za kila siku. Kila mtu ana kiwango chake cha maji kinachohitajika kwa siku. Unaweza kujua kiwango chako cha maji kinachohitajika kwa siku kwa kuzungumza na daktari wako.” image-1=”” headline-2=”h3″ question-2=”Je, ni Njia ipi bora ya kunywa maji?” answer-2=”Ni bora kunywa maji kidogo kidogo kwa vipindi virefu badala ya kunywa maji yote kwa wakati mmoja. Pia, ni bora kunywa maji kwa saa moja au mbili baada ya kula.” image-2=”” count=”3″ html=”true” css_class=””]

Hitimisho

Kunywa maji mengi ni muhimu kwa afya yako, lakini unapaswa kuzingatia kunywa maji kwa kiwango kinachohitajika na kuzingatia vidokezo vya kuzuia madhara kutokea,

Kwa kufanya hivyo, unaweza kufurahia faida za kunywa maji bila kusababisha madhara yoyote kwenye mwili wako.

Ni muhimu kuzingatia kwamba kila mtu ana kiwango chake cha maji kinachohitajika kwa siku na unapaswa kuzungumza na daktari wako ili kujua kiwango chako cha maji kinachohitajika kwa siku.

Kwa kumalizia, unaweza kuendelea kufurahia faida za kunywa maji kwa kuzingatia vidokezo hivi. Ni muhimu pia kuepuka kunywa maji kupita kiasi ili kuepuka madhara yoyote ya kiafya.

SUMMARY

Haya ni baadhi ya Madhara ya Kunywa Maji mengi Kupita Kiasi;

  1. Kupata hali ya Kichefuchefu na Kutapika
  2. Kupata Maumivu ya kichwa mara kwa mara
  3. Kuvimba Miguu,Mikono au lips za mdomo
  4. Misuli ya mwili kuwa dhaifu na kupata shida ya kukaza na kukakamaa kwa urahisi(cramps), hii ni kutokana na kushuka kwa kiwango cha baadhi ya Electrolyte mwilini
  5. Mwili kuchoka kupita Kiasi(Fatique), Hali hii hutokana na FIGO zako kufanya kazi kupita kiasi wakati wa kutoa kiwango kinachozidi  mwilini, matokeo yake husababisha hormones reactions ambazo huleta hali ya Msongo wa mawazo,Uchovu wa mwili n.k

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In https://afyaclass.com Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 months ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa3 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa3 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa5 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake5 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa4 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa2 days ago

kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani

kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani Unapopata tatizo la kuharisha na kutapika kwa wakati mmoja unaweza kuwaza sana,...

Magonjwa4 days ago

Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu

Dalili za infection kwenye damu Mchafuko wa damu,chanzo,dalili na Tiba Mchafuko wa damu; hiki ni kiswahili ambacho watu wamezoea kukitumia...

Magonjwa7 days ago

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri Yapo magonjwa mbali mbali ya ngozi ambayo huweza kuathiri Sehemu za Siri za Mwanaume...

Magonjwa2 weeks ago

Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu

Dalili za acid reflux: Tatizo la Gastroesophageal reflux disease (GERD), ni tatizo ambalo huwapata Watu wengi,Tatizo hili hujulikana kwa jina...

Magonjwa4 weeks ago

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe au ni ugonjwa ambao huhusisha ngozi kupoteza rangi...

Magonjwa4 weeks ago

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni,...

Magonjwa1 month ago

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu Utangulizi: Scabies huhusisha mtu kuwa na vipele na muwasho kwenye ngozi yake ambapo...

Magonjwa1 month ago

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume Gono ni neno maarufu ambalo kirefu chake ni Gonorrhea na kiswahili chake ni...

Magonjwa1 month ago

Dalili Mpya za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni Dalili za ukimwi kwenye ngozi Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala...

Magonjwa1 month ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Trending