Magonjwa
vyakula vya mama anayenyonyesha,Soma zaidi hapa kufahamu
vyakula vya mama anayenyonyesha,Soma zaidi hapa kufahamu
Ni muhimu sana kwa mama anayenyonyesha kufahamu kuhusu Lishe bora katika kipindi hiki, kwani Lishe bora kwake ni msaada hata kwa Mtoto wake anayenyonya,
mfano: Moja ya vyakula vya mama anayenyonyesha ni pamoja na vyakula vyenye Vyanzo vya protini kwa wakina mama wanaonyonyesha, n.k
Kwa kulitambua hilo,katika Makala hii tumechambua baadhi ya vyakula vya mama anayenyonyesha ili kumsaidia yeye pamoja na mtoto wake;
vyakula vya mama anayenyonyesha
Soma hapa kufahamu baadhi ya vyakula vya mama anayenyonyesha;
1. Unahitajika kula zaidi kidogo ukilinganisha na mama ambaye hanyonyeshi, ili upate nguvu za kutosha pamoja na Virutubisho kwa ajili ya kuzalisha Maziwa zaidi,
Unahitaji ongezeko la Calories 330 mpaka 400 calories kwa Siku, ili kukupa nguvu(energy) pamoja Virutubisho(nutrition) ili kuzalisha Maziwa zaidi.
Hivo ili kupata extra calories, lazima ule vyakula vyenye wingi wa Virutubisho hivo, kama vile;
- kipande cha mkate wa nafaka nzima
- na kijiko kikubwa (karibu gramu 16) cha siagi ya karanga,
- ndizi kiasi
- Pamoja na karibu gramu 227 za mtindi(yogurt)
Hivo basi, hivi ni baadhi ya vyakula vya mama anayenyonyesha
2. Kula Vyakula ambavyo vitasaidia kuzalisha Maziwa mengi Zaidi na yenye ubora,
Miongoni mwa vyakula vya mama anayenyonyesha ni pamoja na vyakula vya kumsaidia azalishe Maziwa mengi Zaidi,
Hapa nazungumzia vyakula vyenye Vyanzo vya protini kwa wakina mama wanaonyonyesha, mfano;
- nyama,
- mayai,
- maziwa,
- maharagwe,
- dengu
- Pamoja na vyakula vya baharini(seafood) kama vile Samaki,dagaa ambazo hazina zebaki. n.k.
Pia usisahau kula Matunda Pamoja na mboga za Majani.
3. Kula vyakula tofauti tofauti wakati wa Kunyonyesha,
hii inaweza Kusaidia kubadilisha ladha ya Maziwa, na kumfanya mtoto kupata ladha tofauti tofauti, hali ambayo itamsaidia kutokupata shida hata itakapofikia hatua ya kumpa vyakula tofauti tofauti.
4. Moja ya vyakula vya mama anayenyonyesha ni pamoja na vyakula vyenye kiwango cha kutosha cha Vitamins,
kama vile mboga za Majani n.k
5. Hakikisha unakunywa Maji ya kutosha
6. Epuka vyakula vyenye kiwango kikubwa cha Sukari,Chumvi, pamoja na vinywaji vyenye Caffeine nyingi,
7. Hakikisha vyakula vya mama anayenyonyesha vina Virutubisho hivi muhimu;
- Madini chuma,
- Proteins,
- Pamoja na Calcium,
• Vyanzo bora vyenye Madini chuma ni pamoja na;
- Samaki
- Dagaa
- nyama
- nafaka- enriched cereals,
- mboga za majani-leafy green vegetables,
- peas,
- pamoja na matunda yaani dried fruit kama vile raisins. n.k
Pia kula vyakula vyenye Kiwango kikubwa cha Vitamin C ili kusaiida ufyozwaji mzuri wa madin chuma, hivo tumia vitu kama matunda ambayo ni jamii ya Citrus fruits kama vile machungwa n.k
• Vyakula bora vyenye Proteins ni pamoja na;
- nyama,
- mayai,
- maziwa,
- maharagwe,
- dengu
- Pamoja na vyakula vya baharini(seafood) kama vile Samaki,dagaa ambazo hazina zebaki. n.k.
• Vyakula bora vyenye Calcium ni pamoja na;
- Maziwa ya ng’ombe-cow’s milk au vitu vyovyote vyenye maziwa ndani yake yaani dairy products
- Kula mboga za majani-dark green vegetables.
- Pamoja na vitu vingine kama vile juices, nafaka(cereals), soy milk, n.k
8. Pia unaweza kupata Virutubisho mbali mbali(supplements).
Hasa vyenye Vitamins kama vile vitamin B-12 supplement n.k.
9. Epuka kabsa matumizi ya Pombe, hakuna kiwango Sahihi cha pombe kwa mama anayenyonyesha,
hivo acha kabsa kutumia Pombe kama unanyonyesha kwa ajili ya afya yako na mtoto wako.
10. Epuka kunywa Vinywaji vyenye kiwango kikubwa cha Caffeine,
Epuka kunywa zaidi ya vikombe 2 mpaka 3 vya kahawa kwa siku.
FAQs; Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
Je, Mama anayenyonyesha anaruhusiwa kunywa Pombe?
Hapana, hakuna kiwango sahihi cha pombe ambacho kinaruhusiwa kwa mama anayenyonyesha, acha kabsa pombe kama unanyonyesha.
je, vyakula vya mama anayenyonyesha ni vipi?
Vyakula bora kwa mama anayenyonyesha ni pamoja na vyakula vyenye wingi wa proteins,madini chuma, calcium,vitamins, n.k
Hitimisho
Ni muhimu sana kufahamu vyakula vya mama anayenyonyesha, hii itakusaidia kuzalisha maziwa mengi zaidi na kwa ubora unaohitajika kwa afya yako pamoja na mtoto wako,
epuka tabia hatarishi kama vile; kunywa pombe,kuvuta Sigara, kutumia dawa hovio pasipo maelekezo kutoka kwa wataalamu wa afya, au Imani potofu kama za kupaka baadhi ya dawa kwenye chuchu n.k
kwa kuzingatia haya,tutajenga afya bora kwa mama na mtoto pia.
Hivo basi, Zingatia vyakula vya mama anayenyonyesha, Soma zaidi ili kufahamu.
AU KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.
-
Uzazi/Ujauzito5 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Magonjwa4 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Uzazi/Ujauzito3 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa7 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Magonjwa2 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events6 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News4 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
Utafiti22 hours ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO