Connect with us

Magonjwa

TATIZO LA KUUMWA UBAVU WA KUSHOTO WAKATI WA KULALA

Avatar photo

Published

on

Kuna wakati maumivu haya ya ubavu wa kushoto hasa wakati wa kulala huisha yenyewe kulingana na chanzo chake,ila kuna wakati linakuwa ni tatizo la muda mrefu ambalo huhitaji Tiba kamili,katika makala hii tumechambua kuhusu vyanzo mbali mbali vya tatizo hili pamoja na Tiba yake.

CHANZO CHA TATIZO LA KUUMWA UBAVU WA KUSHOTO WAKATI WA KULALA

kuna sababu mbali mbali ambazo huweza kupelekea mtu kupatwa na tatizo hili la maumivu makali ya ubavu wa kushoto wakati wa kulala na sababu hizo ni kama vile;

1. Tatizo la kuvimba,kuharibiwa au kupasuka kwa bandama au wengu huweza kusababisha matatizo mbali mbali kwa mgonjwa ikiwemo; kupata maumivu makali ubavu wa kushoto,kupata kizunguzungu,kutokuona vizuri,mgonjwa kuchoka sana,kichefuchefu n.k

Kuvimba kwa bandama au wengu huweza kuchangiwa na sababu mbali mbali kama vile; maambukizi ya virusi kama mononucleosis,maambukizi ya bacteria kama kaswende(syphilis), maambukizi ya parasite kama Malaria,magonjwa ya ini,damu n.k

2. Kupatwa na tatizo la kuvunjika kwa mbavu au kupata majeraha kwenye mbavu kutokana na sababu mbali mbali kama vile ajali,kuanguka n.k

3. Tatizo la Costochondritis, hili ni tatizo ambalo huhusisha kuvimba kwa gegedu yaani Cartilage ambazo zimejishikiza kwenye mbavu hasa upande wa kushoto,kuvimba kwa cartilage hizo hutokana na sababu mbali mbali ikiwemo; maambukizi ya vimelea vya magonjwa,kuumia,tatizo la arthritis n.k

4. Tatizo la kuvimba kwa kongosho yaani pancreatitis, Mtu mwenye shida hii huanza kupata maumivu taratibu ambayo huongezeka kadri siku zinavyokwenda hasa baada ya kula chakula, kuvimba kwa kongosho huweza kutokana na sababu kama vile; kuumia,matumzi ya pombe kupita kiasi,tatizo la gallstones n.k

5. Tatizo la kuvimba kwa kuta za tumbo yaani Gastritis, hasa kwenye eneo la upande wa kushoto karibu kabsa na mbavu zako,tatizo hili huweza kusababisha maumivu makali ya ubavu wa kushoto hasa wakati wa kulala,

Kuvimba kwa kuta za tumbo huweza kutokana na sababu mbali mbali kama vile; maambukizi ya bacteria au virusi,matumizi ya pombe kupita kiasi,matumizi ya dawa jamii ya nonsteroidal anti inflammatory(NSAIDs) kwa kiasi kikubwa n.k

6. Maambukizi kwenye figo au tatizo la mawe kwenye figo(kidney stones), watu wenye shida hii huweza kupata tatizo la maumivu ya ubavu wa kushoto pia

7. Kuvimba kwa pericardium kutokana na sababu mbali mbali kama vile maambukizi ya magonjwa,kuumia,matumizi ya dawa jamii ya anti-seizures kwa kiasi kikubwa n.k

8. Tatizo la kuvimba kwa tissue zinazofunika mapafu yaani Pleurisy, kutokana na sababu mbali mbali kama vile kuumia,maambukizi ya magonjwa, Bacteria,virusi,fungal pneumonia n.k

9.Lakini pia mtu huweza kupata maumivu ya ubavu wa kushoto baada ya kulala vibaya,japo maumivu haya hayawezi kudumu kwa muda mrefu sana.

DALILI ZA HATARI KWA MTU MWENYE MAUMIVU MAKALI YA UBAVU WA KUSHOTO

Muone daktari haraka Endapo unapata maumivu makali ya ubavu wa kushoto lakini yanaambatana na:

– Tatizo la kushindwa kupumua au kukosa pumzi

-Tatizo la kutokwa na jasho kupita kiasi

– Maumivu makali ya kichwa

– Kupatwa na kizunguzungu kikali

– Mtu kuonyesha dalili zote za kuchanganyikiwa n.k

VIPIMO

Mtu mwenye tatizo la maumivu ya ubavu wa kushoto huweza kupimwa kwa;

• kuangaliwa na kuminywa sehemu ya tatizo yaani physical examination

• Kipimo cha Electrocardiogram

• Vipimo vya damu pamoja na mkojo

• X-ray, CT scan au MRI

MATIBABU YA TATIZO LA KUUMWA UBAVU WA KUSHOTO WAKATI WA KULALA

Tiba ya tatizo hili hutegemea na chanzo husika,hivo kama chanzo ni kuvimba basi mgonjwa atapewa dawa jamii ya nonsteroidal anti inflammatory drugs(NSAIDs) kupunguza maumivu pamoja na uvimbe, kama tatizo ni maambukizi ya bacteria mgonjwa atapewa antibiotics mbali mbali n.k

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In https://afyaclass.com Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 months ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa3 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa3 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa5 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake5 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa4 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa2 days ago

kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani

kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani Unapopata tatizo la kuharisha na kutapika kwa wakati mmoja unaweza kuwaza sana,...

Magonjwa4 days ago

Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu

Dalili za infection kwenye damu Mchafuko wa damu,chanzo,dalili na Tiba Mchafuko wa damu; hiki ni kiswahili ambacho watu wamezoea kukitumia...

Magonjwa7 days ago

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri Yapo magonjwa mbali mbali ya ngozi ambayo huweza kuathiri Sehemu za Siri za Mwanaume...

Magonjwa2 weeks ago

Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu

Dalili za acid reflux: Tatizo la Gastroesophageal reflux disease (GERD), ni tatizo ambalo huwapata Watu wengi,Tatizo hili hujulikana kwa jina...

Magonjwa4 weeks ago

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe au ni ugonjwa ambao huhusisha ngozi kupoteza rangi...

Magonjwa4 weeks ago

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni,...

Magonjwa1 month ago

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu Utangulizi: Scabies huhusisha mtu kuwa na vipele na muwasho kwenye ngozi yake ambapo...

Magonjwa1 month ago

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume Gono ni neno maarufu ambalo kirefu chake ni Gonorrhea na kiswahili chake ni...

Magonjwa1 month ago

Dalili Mpya za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni Dalili za ukimwi kwenye ngozi Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala...

Magonjwa1 month ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Trending