Connect with us

Magonjwa

TATIZO LA USONJI(AUTISM),CHANZO,DALILI NA TIBA YAKE

Avatar photo

Published

on

Tatizo la usonji(autism) ni tatizo ambalo huhusisha hitilafu kwenye maendeleo ya ubongo wa mtoto ambayo huleta shida zingine kama vile; tatizo la mtoto kutokuongea,kujitenga n.k,na tatizo hili huanzia utotoni na kusababisha matatizo makubwa mpaka utu uzima.

Tatizo hili la Usonji ambapo kwa kitaalam hujulikana kama Autism hutokea kwa baadhi ya watoto na tafiti zinaonyesha kwa wazazi wengi huchelewa kugundua kama watoto wao wana shida hiyo mpaka watoto wakiwa na umri wa miaka 2-3 na kuendelea.

Mtoto mwenye tatizo la Usonji hupatwa na tatizo la kutokuongea,hupenda kujitenga sana na wenzake au watu wengine, na pia tafiti zinaonyesha kwamba tatizo hili la Usonji huwapata watoto wa jinsia ya KIUME zaidi kuliko ya KIKE.

CHANZO CHA TATIZO LA USONJI

– Mpaka sasa hakuna sababu ya moja kwa moja ya kutokea kwa tatizo la Usonji au Autism,japo kuna baadhi ya sababu ambazo zimeonekana kuweza kuchangia kwa kiasi kikubwa kutokea kwa tatizo hili la Usonji,na sababu hizo ni kama vile;

1. Tatizo la vinasaba(genetics) ambapo hujulikana kwa kitaalam kama vile neurodevelopmental disorders, hapa tunazungumzia matatizo mbali mbali kama vile Rett syndrome,Fragile X syndrome n.k

2. Sababu za kimazingira kama vile; Kupatwa na maambukizi ya (Virusi) ugonjwa wa RUBELLA n.k

3. Matumizi ya baadhi ya dawa kipindi cha ujauzito

4. Complications mbali mbali ambazo huweza kumpata mama wakati wa ujauzito

5. Mama mjamzito kutumia vilevyi mbali mbali kama vile pombe,madawa ya kulevyia kama Coccaine n.k

6. Uchafuzi wa hewa hivo kusababisha watu kuvuta hewa chafu n.k

7. Kuwa na mtoto mwenye tatizo hili la usonji kwenye familia au koo flani huweza kuongeza uwezekano wa watoto wengine kuzaliwa na tatizo hili

8. Mtoto kuzaliwa kabla ya wakati hasa kama imetokea kabla ya wiki 26 za ujauzito, na kwa hapa kwetu Tanzania ni ngumu sana kwa mtoto huyu kuishi,angalau kuanzia wiki 28 na kuendelea uwezekano wa kuishi ni mkubwa.

9. Wazazi kujifungua watoto wakiwa na umri mkubwa sana,japo tafiti zinaendelea kufanyika juu ya hili,ila baadhi ya tafiti zinasema mwanamke kuchelewa kuzaa au kuzaa akiwa na umri mkubwa sana huweza kuchangia uwepo wa tatizo hili la Usonji

NJIA ZA UTAMBUZI WA TATIZO HILI KWA MTOTO

• Wataalam wa afya watataka kujua kuhusu hatua za ukuaji wa mtoto,uwezo wake wa akili pamoja na kufanya vipimo mbali mbali kama vile genetic testing n.k

DALILI ZA TATIZO LA USONJI NI PAMOJA NA;

– Mtoto kushindwa kuitika baada ya kuitwa jina lake au mtoto kuonekana kutokusikia kabsa wakati akiitwa jina lake

– Mtoto kushindwa kutazama watu usoni(eye contacts), kutokucheka,n.k

– Mtoto kutokuongea kabsa au kuchelewa sana kuongea kuliko kawaida

– Kupoteza uwezo wa kutamka maneno au sentensi ambazo mwanzoni alikuwa anaweza kutamka

– Mtoto kushindwa kabsa kuanzisha mazungumzo

– Mtoto kuongea huku akitoa sauti zisizozakawaida

– Mtoto kushindwa kuelewa maswali rahisi akiulizwa na watu

– Mtoto kufanya vitu vya kujidhuru mwenyewe kama vile; kujipiga mwenyewe,kujibamiza kichwa n.k

– Mtoto kutokutaka mwanga,kushtuka sana akiguswa au kusikia sauti yoyote

– Mtoto kutokutamka maneno ya kitoto mpaka afikishe umri wa mwaka mmoja na kuendelea

– Mtoto kutokuongea neno lolote mpaka afikishe kipindi cha umri wa miezi kumi na sita

– Mtoto kupoteza kabsa uwezo wake wa kuongea

– Mtoto kushindwa kufanya vitu mbali mbali kama kupunga mkono kwa wazazi au mtu yoyote kama ishara ya kumsalimia au kumuaga mpaka anapofikisha kipindi cha umri wa miezi kumi na mbili

– Mtoto kushindwa kuongea maneno zaidi ya mawili au sentensi ya maneno mpaka anapofikisha umri wa miezi 24

– Mtoto kuwa na tabia ya kukaa peke yake pamoja na kujitenga na watu N.k

MADHARA YA TATIZO LA USONJI KWA WATOTO NI PAMOJA NA;

• Mtoto kushindwa kuongea kabsa,kuchelewa sana kuongea au kuongea maneno ambayo hayaeleweki

• Mtoto kushindwa kuchangamana na watu wengine(kujitenga muda wote)

• Mtoto kuwa na matatizo ya kutokuelewa akiwa shuleni

• Tatizo la kupewa ajira au kuajiriwa

• Kusababisha msongo wa mawazo na hali ya huzuni katika familia N.k

MATIBABU YA TATIZO LA USONJI

Tatizo hili halitibiki au hakuna tiba ya kuondoa kabsa tatizo hili,ila kuna tiba ya kudhibiti dalili mbali mbali ambazo husababishwa na tatizo hili la Usonji, na kwa ujumla wake zipo tiba mbali mbali kama vile;

✓ Matumizi ya dawa za kudhibiti dalili za tatizo la Usonji

✓ Huduma ya kimawasiliano pamoja na ufundishwaji wa tabia mbali mbali kwa mtoto yaani Behavior and Communication therapy

✓ Huduma ya uelimishwaji yaani educational therapy n.k

 

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In https://afyaclass.com Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 months ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa3 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa3 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa5 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake5 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa4 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu

Dalili za infection kwenye damu Mchafuko wa damu,chanzo,dalili na Tiba Mchafuko wa damu; hiki ni kiswahili ambacho watu wamezoea kukitumia...

Magonjwa4 days ago

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri Yapo magonjwa mbali mbali ya ngozi ambayo huweza kuathiri Sehemu za Siri za Mwanaume...

Magonjwa1 week ago

Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu

Dalili za acid reflux: Tatizo la Gastroesophageal reflux disease (GERD), ni tatizo ambalo huwapata Watu wengi,Tatizo hili hujulikana kwa jina...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe au ni ugonjwa ambao huhusisha ngozi kupoteza rangi...

Magonjwa4 weeks ago

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni,...

Magonjwa4 weeks ago

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu Utangulizi: Scabies huhusisha mtu kuwa na vipele na muwasho kwenye ngozi yake ambapo...

Magonjwa1 month ago

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume Gono ni neno maarufu ambalo kirefu chake ni Gonorrhea na kiswahili chake ni...

Magonjwa1 month ago

Dalili Mpya za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni Dalili za ukimwi kwenye ngozi Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala...

Magonjwa1 month ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Magonjwa1 month ago

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake Karibu! Hapa kwa makala yenye taarifa muhimu kuhusu...

Trending