Magonjwa
Ugonjwa wa Gambiense Sleeping Sickness,African Trypanosomiasis
![](https://afyaclass.com/mk_omb/uploads/2022/11/200px-PMC5373517_pntd.0005324.g001.png)
Ugonjwa wa Gambiense Sleeping Sickness,African Trypanosomiasis,chanzo,dalili na Tiba yake
Ugonjwa huu hujulikana kama African Trypanosomiasis au kwa Jina lingine “sleeping sickness”
Jina la African Trypanosomiasis ni kwa sababu ya Ugonjwa huu kuwepo Afrika Hasa sub-Saharan Africa,
CHANZO CHA UGONJWA HUU NI NINI?
Ugonjwa huu husababishwa na parasites wadogo sana kutoka kwenye jamii ya Trypanosoma brucei,
Kisha kusambazwa na tsetse fly (Glossina species),
Wanyama wa kufugwa na wanyama wa msituni huweza kuhifadhi Parasite hawa, wanyama hao ni kama Nguruwe, Mbwa,mbuzi, n.k
Na pia Binadamu anaweza kuwa Main reservoir wa Infection hii.
Kuna Species mbili za Trypanosoma brucei;
(1)Trypanosoma brucei-gambiense
(2) Trypanosoma brucei-rhodesiense
T. b. gambiense wanasababisha African trypanosomiasis hasa kwenye eneo la western na central Africa wakati T. b. rhodesiense husababisha African trypanosomiasis hasa hasa kwenye eneo la eastern na southern Africa.
DALILI ZA UGONJWA HUU WA SLEEPING SICKNESS
Ugonjwa huu umepewa jina la Sleeping sickness kwa Sababu Dalili zake huweza kujumuisha matatizo ya Usingizi,
– Baada ya Mtu kung’atwa na tsetse fly anaweza kupata maumivu kisha kuwa na kidonda chekundu(red sore) ambacho huitwa chancre.
– Mtu kupata homa
– Mtu kupata maumivu makali ya Kichwa
– Mwili kutokutulia(irritability)
– Mtu kupata uchovu usio wa kawaida
– Mara nyingi Mtu wenye Ugonjwa huu wa Sleeping sickness hupata maumivu ya Misuli Pamoja na Joints
– Baadhi ya watu hupata vipele kwenye ngozi au Skin rashes
– Mtu kuwa kama amechanganyikiwa
– Wagonjwa wachache huweza Kuvimba Uso
– Na kama mgonjwa hajapata Tiba maambukizi haya huweza kuwa makali zaidi na kusababisha Kifo
MATIBABU YA UGONJWA HUU WA SLEEPING SICKNESS
Matibabu ya Ugonjwa huu hutegemea na aina ya maambukizi(T. b. gambiense au T. b. rhodesiense) pamoja na hatua ya Ugonjwa ulipofikia.
Dawa kama Pentamidine,suramin, melarsoprol, eflornithine, nifurtimox huweza kutumika.
-
Magonjwa5 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Uzazi/Ujauzito3 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Magonjwa2 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Uzazi/Ujauzito1 day ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Events4 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News3 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
Magonjwa3 hours ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani