Magonjwa
Ugonjwa wa pid kwa mwanaume,Je wanaume wanaweza kuwa na PID?
Ugonjwa wa pid kwa mwanaume,Je wanaume wanaweza kuwa na PID?
Moja ya Maswali ambayo watu wengi wamekuwa wakiuliza ni kuhusu mwanaume kupata Ugonjwa wa Pid, je inawezekana?
Hapana, Mwanaume hawezi kuwa na Ugonjwa wa PID(Pelvic inflammatory disease),
Hii n kwa Sababu PID ni ugonjwa ambayo huhusisha maambukizi ya vimelea vya magonjwa kama vile bacteria kwenye Via vya Uzazi vya Mwanamke,
Kwa Ujumla,Ugonjwa huu wa PID hushambulia mfumo wa Uzazi kwa mwanamke, ikiwa ni Pamoja na;
- Kizazi(Uterus)
- Mirija ya uzazi(fallopian tubes)
- au Vifuko vya Mayai(Ovaries)
PID hutokea wakati bacteria wakipanda kutoka Ukeni kwenda kwenye viungo vya juu vya uzazi, au tunasema upper reproductive organs.
Mara nyingi, bakteria hawa huambukizwa kwa ngono, na magonjwa ya zinaa kama kisonono na chlamydia yanaweza kusababisha PID.
Fahamu pia, inawezekana kwa wanaume kuwa na magonjwa hayo ya Zinaa(Kisonono,chlamydia), na wanaweza kueneza bakteria wanaohusika kuyaeneza kwa mwanamke,
Hivo kumuweka mwanamke kwenye hatari zaidi ya kupata magonjwa haya ya zinaa ambayo pia huweza kupelekea Mwanamke kupata PID.
Hata hivyo, haiwezekani kwa Magonjwa haya ya Zinaa kusababisha PID kwa wanaume kama inavyoweza kutokea kwa wanawake.
Vitu vya Kuzingatia ni pamoja na;
• Mwanaume kupata Tiba endapo ana magonjwa haya ya Zinaa
• Mwanaume kupata Tiba hata kama haumwi,pale ambapo Mke wake au mwezi wake amagendulika ana Ugonjwa wa PID.
• Mwanamke,Wapenzi wowote ambao umekuwa nao kwa muda wa miezi 6 kabla ya dalili zako kuanza wanapaswa kupimwa na kutibiwa ili kuzuia maambukizi kujirudia au kuenea kwa wengine.
Dalili za Ugonjwa wa PID
Dalili za Ugonjwa wa PID ni Pamoja na;
1. Kupata maumivu karibu na eneo la nyonga au tumbo chini ya kitovu
2. Kupata maumivu wakati wa tendo la ndoa
3. Kupata maumivu wakati wa kukojoa
4. kutokwa na damu katikati ya mwezi kabla hedhi na baada ya tendo la ndoa
5. Kupata damu nzito au nyingi wakati wa hedhi(heavy periods)
6. Kupata maumivu makali sana wakati wa hedhi
7. Kutokwa na uchafu ukeni wenye rangi ya njano au kijani ambao huambatana na harufu mbaya.
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.
-
Uzazi/Ujauzito5 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Magonjwa4 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Uzazi/Ujauzito3 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa7 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Magonjwa2 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events6 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News4 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
Utafiti21 hours ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO