Magonjwa
Vipimo Vya Saratani ya Matiti, shingo ya kizazi, Utumbo mpana pamoja na saratani ya Mapafu
Cancer Screening tests inamaanisha kuangalia mwili wako ili kubaini saratani kabla ya kuwa na dalili na hata baada ya kuonyesha dalili. Kupata vipimo vya uchunguzi mara kwa mara kunaweza kubaini kama una saratani ya matiti, shingo ya kizazi, na utumbo mpana mapema zaidi.
Ikiwa umegundua Saratani mapema matibabu yana uwezekano wa kufanya kazi vyema zaidi. Uchunguzi wa saratani ya mapafu unapendekezwa kwa baadhi ya watu walio katika hatari kubwa.
Saratani ya matiti
Mammograms ndio njia bora ya kusaidia kubaini kama una saratani ya matiti. Ambapo ni rahisi kutibu kabla haijafikia kwenye kiwango kikubwa cha kutosha kuhisi au kusababisha dalili.
Saratani ya Shingo ya Kizazi
Kipimo cha Pap kinaweza kupata seli zisizo za kawaida kwenye shingo ya kizazi ambazo zinaweza kugeuka kuwa saratani. Kipimo cha HPV (human papilloma virus) huweza kusababisha mabadiliko haya ya seli. Vipimo vya Pap pia vinaweza kupata saratani ya shingo ya kizazi mapema, wakati uwezekano wa kuponywa ni mkubwa sana.
NB: Mpango wa Kitaifa wa Uchunguzi wa Mapema wa Saratani ya Matiti na Shingo ya Kizazi wa CDC unatoa vipimo vya mammogramu na Pap bila malipo au vya gharama nafuu nchini kote.
Saratani ya utumbo mpana(colon cancer)
Saratani ya utumbo mpana karibu kila mara hukua kutokana na polipu (precancerous polyps) kwenye koloni au rektamu.Vipimo vya uchunguzi vinaweza kupata polyps zisizo na saratani, kwa hivyo zinaweza kuondolewa kabla hazijageuka kuwa saratani,Vipimo vya uchunguzi pia vinaweza kugundua Pale seli zinapogeuka kuwa saratani ya utumbo mpana, wakati matibabu yanafanya kazi vyema zaidi endapo saratani imebainika ikiwa kwenye hatua za mwanzoni.
Saratani ya mapafu
USPSTF inapendekeza uchunguzi wa kila mwaka wa saratani ya mapafu kwa kutumia dozi ya chini ya tomografia ya kompyuta (LDCT)low-dose computed tomography kwa watu ambao wana historia ya kuvuta sigara nyingi, na wanaovuta sigara sasa au wale ambao wameacha ndani ya miaka 15 iliyopita, na wana umri wa kati ya miaka 50 na 80.
-
Uzazi/Ujauzito5 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Magonjwa4 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Uzazi/Ujauzito3 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa7 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Magonjwa2 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events6 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News4 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
Utafiti22 hours ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO