News
TAKWIMU mpya: Idadi ya magonjwa ya Zinaa kuongezeka nchini, Wanawake waathiriwa Zaidi
TAKWIMU mpya: Idadi ya magonjwa ya Zinaa kuongezeka nchini, Wanawake waathiriwa Zaidi.
Kushamiri kwa ngono zembe miongoni mwa watu nchini kunatajwa kusababisha kuongezeka kwa idadi ya magonjwa ya ngono, hasa kwa wanawake.
Takwimu za Ripoti ya Utafiti wa Afya ya Uzazi, Mtoto na Viashiria vya Malaria nchini ya mwaka 2022 (TDHS-MIS 2022) iliyotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kwa kushirikiana na Wizara ya Afya zinaonyesha asilimia 14 ya wanawake wana magonjwa yanayoambukizwa kwa ngono, ikiwa ni ongezeko kutoka asilimia saba mwaka 2010.
Wakati maambukizi ya magonjwa hayo yakiongezeka kwa asilimia saba kwa wanawake na asilimia saba nyingine kwa wanaume mwaka 2022 ikilinganishwa na mwaka 2010, Mkoa wa Katavi unatajwa kuwa kinara, hususan kwa wanawake wenye tatizo hilo kwa asilimia 11.4.
Rukwa inafuatia kwa kuwa na wanawake wenye maambukizi hayo kwa asilimia 11, huku Shinyanga ikishika nafasi ya tatu kwa kuwa na maambukizi ya asilimia 9.1.
Kilimanjaro unafuatia kwa kuwa na asilimia 9.5 na Dar es Salaam inafunga orodha hiyo kwa kuwa na maambukizi ya asilimia 9.1.
Takwimu hizo zinaonesha katika mikoa hiyo mitano, mwanamke mmoja kati ya 10 ana maambukizi ya magonjwa ya ngono yanayotajwa kuwa miongoni mwa viashiria vya virusi vya Ukimwi.
-
Uzazi/Ujauzito6 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Uzazi/Ujauzito4 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa5 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Magonjwa3 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events7 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News5 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
afyatips19 hours ago
Madhara ya damu kuwa nyingi mwilini
-
Utafiti2 days ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO