Connect with us

News

Miili ya watoto wawili kufanyiwa vipimo vya DNA Hanang

Avatar photo

Published

on

Miili ya watoto wawili kufanyiwa vipimo vya DNA Hanang

Maporomoko ya tope, magogo, mawe, maji na miti yalitokea alfajiri ya Desemba 2, 2023 katika Mji Mdogo wa Katesh, wilayani Hanang.

Dar es Salaam. Serikali imesema miili ya watoto wawili wa kike wa mwaka mmoja na miaka mitatu iliyoopolewa kwenye maporomoko ya tope mkoani Manyara, inafanyiwa vipimo vya vinasaba (DNA) ili kujiridhisha na utambuzi wake.

Vifo vya watu 87 vimethibitishwa na Serikali na miili ya wahusika imeshatambuliwa na kuchukuliwa na familia zao.

Hayo yameelezwa na Msemaji wa Serikali, Mobhare Matinyi kupitia taarifa aliyoitoa kwa umma leo Desemba 13,2023.

“Bado utafutaji unaendelea. Serikali inaendelea kugharamia mazishi na kutoa mkono wa pole wa Sh1 milioni kwa kila mwili kwa agizo la Rais Samia Suluhu Hassan,” amesema.

Kuhusu majeruhi, Matinyi amesema idadi inaendeelea kupungua na hadi kufikia saa tisa alasiri ya leo Desemba 13,2023 wamebakia  15 kutoka 139 waliofikishwa hospitalini na kupatiwa matibabu.

Amesema katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Manyara majeruhi wapo tisa, Hospitali ya Wilaya ya Hanang (Tumaini) wapo watatu, na Kituo cha Afya Gendabi, watatu. Matibabu ya majeruhi wote yanagharamiwa na Serikali.

Kuhusu waathirika walio kwenye makambi, Matinyi amesema wamebaki 96 ambao Serikali inaendelea kuwaunganisha na ndugu zao.

Amesema kila kaya inayoondoka inapewa chakula na mahitaji muhimu ya kuwasaidia kuendelea na maisha.

“Hadi sasa waathirika 438 wa kaya 119 wameunganishwa na ndugu na jamaa zao. Kuna mchakato wa kuziunganisha na ndugu zao kaya zingine 31 zenye watu 96,” amesema.

Matinyi amesema Serikali kupitia Wizara ya Afya inaendelea kusimamia suala la afya kwa umma,  na kuhakikisha magonjwa ya mlipuko hayatokei katika eneo lote lililoathirika na maafa.

Amesema juhudi hizo zinahusisha kuzitembelea kaya, na hadi sasa kaya 5,410 zimeshafikiwa na dawa 102,405 za kutibu maji zimeshagawiwa.

“Waathirika wengine 1,853  wameshapatiwa msaada wa kisaikolojia na timu ya wataalamu wa Wizara ya Afya, wakiwamo wauguzi wawili, madaktari bingwa watatu wa afya ya akili na maofisa ustawi wa jamii 91 kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu,” amesema.

Kwa wanaotaka kutoa msaada, amesema Kamati ya Maafa ya Taifa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, imetoa akaunti ya benki ya kutuma fedha kwa mujibu wa Sheria ya Usimamizi wa Maafa Na. 6 ya mwaka 2022.

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa3 months ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa3 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa3 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa5 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake5 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

magonjwa ya wanaume4 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa3 days ago

kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani

kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani Unapopata tatizo la kuharisha na kutapika kwa wakati mmoja unaweza kuwaza sana,...

Magonjwa5 days ago

Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu

Dalili za infection kwenye damu Mchafuko wa damu,chanzo,dalili na Tiba Mchafuko wa damu; hiki ni kiswahili ambacho watu wamezoea kukitumia...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri Yapo magonjwa mbali mbali ya ngozi ambayo huweza kuathiri Sehemu za Siri za Mwanaume...

Magonjwa2 weeks ago

Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu

Dalili za acid reflux: Tatizo la Gastroesophageal reflux disease (GERD), ni tatizo ambalo huwapata Watu wengi,Tatizo hili hujulikana kwa jina...

Magonjwa4 weeks ago

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe au ni ugonjwa ambao huhusisha ngozi kupoteza rangi...

Magonjwa4 weeks ago

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni,...

Magonjwa1 month ago

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu Utangulizi: Scabies huhusisha mtu kuwa na vipele na muwasho kwenye ngozi yake ambapo...

Magonjwa1 month ago

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume Gono ni neno maarufu ambalo kirefu chake ni Gonorrhea na kiswahili chake ni...

Magonjwa1 month ago

Dalili Mpya za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni Dalili za ukimwi kwenye ngozi Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala...

Magonjwa1 month ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Trending