News
Afariki baada ya Upasuaji wa Kuongeza Shepu Uturuki
Afariki baada ya Upasuaji wa Kuongeza Shepu Uturuki.
Mwanamke wa Uingereza aitwaye Demi Agoglia (26) amefariki dunia siku chache baada ya kufanya upasuaji wa kuongeza shepu (BBL) nchini Uturuki, Magazeti ya Uingereza yameripoti.
Demi ambaye alikua Mkazi kutoka Jiji la Manchester alipata mshtuko wa moyo saa chache kabla ya kuanza safari yake ya kurudi nyumbani Uingereza ambapo Mume wake alimpatia huduma ya dharura ya CPR kabla ya kumpeleka Hospitalini lakini jitihada zake hazikuzaa matunda.
Inaelezwa kwamba kiwango cha vifo vinavyotokana na upasuaji wa kuongeza makalio (BBL) ni kifo kimoja kati ya kila Watu 3000 ambapo upasuaji huo wa BBL ndio upasuaji wenye kiwango cha juu zaidi cha vifo vilivyorekodiwa kuliko upasuaji mwingine wowote wa urembo.
Upasuaji wa kuongeza makalio unakadiriwa kugharimu £3,500 (Tsh milioni 11.1) nchini Uturuki lakini hadi £10,000 (Tsh milioni 32) nchini Uingereza huku utafiti ukionesha kuwa ndio upasuaji hatarishi zaidi kuliko upasuaji mwingine wowote wa urembo.
-
Uzazi/Ujauzito5 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Magonjwa4 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Uzazi/Ujauzito3 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa7 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Magonjwa2 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events6 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News4 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
Utafiti23 hours ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO