News
Watu 225 Wafariki Kwa Njaa Huko Tigray, Ethiopia
Watu 225 Wafariki Kwa Njaa Huko Tigray, Ethiopia
ZAIDI ya watu 200 wamekufa kwa njaa tangu Julai katika mji wa Edaga Arbi, katika eneo la Tigray lililokumbwa na ukame na vita, mamlaka za mitaa zilisema.
Wengine 16 wamefariki katika mji wa karibu wa Adwa.
Maafisa huko Tigray wanaonya eneo hilo liko kwenye ukingo wa njaa kwa kiwango cha mwisho kuonekana mnamo 1984, na kusababisha hafla ya kimataifa ya kuchangisha pesa ya muziki Live Aid mwaka uliofuata.
Serikali kuu mjini Addis Ababa inakanusha njaa ipo na kusema inajitahidi kutoa misaada.
Hata hivyo madaktari na wasaidizi wa kibinadamu wanasema misaada haiji haraka vya kutosha, na kuwaacha wakiwa hoi kuokoa maisha.
Wengi wa wanaokufa ni watoto na vijana.
Mkazi wa Tigray Abrehet Kiros anakiambia kituo cha televisheni cha eneo hilo kuwa mara kwa mara humuangalia jirani yake mzee, ambaye hana familia iliyosalia ya kumsaidia baada ya mjukuu wake kufariki katika vita vya wenyewe kwa wenyewe hivi majuzi.
-
Uzazi/Ujauzito5 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Magonjwa4 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Uzazi/Ujauzito3 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa7 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Magonjwa2 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events6 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News5 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
Utafiti23 hours ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO