News
Hamasa ya kujiunga na bima ya afya kwa wote:dkt.mollel
DKT. MOLLEL AOMBA WANANCHI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KATIKA HAMASA YA KUJIUNGA NA BIMA YA AFYA KWA WOTE
Na WAF – Dodoma
Serikali imetoa wito kwa Watanzania, Viongozi wa kisiasa, kidini na kimila kuungana na Serikali katika kuhamasisha umma kujiunga na Bima ya Afya kwa wote pale mchakato utakapoanza rasmi.
Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel wakati akijibu swali namba 56 kwa niaba ya Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu swali la Mheshimiwa Tarimba Gulam Abbas Mbunge wa Jimbo la Kinondoni aliyeuliza Je, nini kauli ya Serikali juu ya Bima ya Afya kwa Watoto?
Dkt. Mollel amesema kuwa nchini kuna watoto Milioni 31, milioni 1.5 wako kwenye mfumo wa Bima ya afya ya sasa na milioni 30.7 wako kwenye mifumo ya bima za afya nyingine zilizopo nchini.
“Niwahakikishie wananchi kuwa ujio wa bima ya afya kwa wote utakuwa suluhisho la changamoto ya matibabu kwa wananchi wote bila kujali hali ya kiuchumi na kikwazo cha fedha, hivyo naomba mchakato utakapoanza wananchi mjitokeze kujiunga na skimu za zitakazobainishwa ambazo zitakua kwa rika zote”. Ameeleza Dkt. Mollel.
-
Uzazi/Ujauzito5 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Magonjwa4 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Uzazi/Ujauzito3 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa7 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Magonjwa2 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events6 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News4 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
Utafiti23 hours ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO