News
SADC yakataa wito wa kutangaza dharura ya afya ya kipindupindu
SADC yakataa wito wa kutangaza dharura ya afya ya kipindupindu
Mawaziri wa afya kutoka muungano wa kanda ya kusini mwa Afrika, Sadc, wamekataa pendekezo la kutangaza kipindupindu kuwa dharura ya afya ya umma katika kanda.
Sylvia Masebo, mwenyekiti wa bodi ya Kituo cha Afrika cha Kudhibiti Magonjwa (CDC), Jumatano alisema nchi moja moja inapaswa kuamua kwa uhuru kama itatangaza mlipuko wa kipindupindu kama dharura ya kiafya au la.
Akizungumza wakati wa kikao cha ajabu cha CDC mjini Addis Ababa, Ethiopia, Bi Masebo, ambaye pia ni waziri wa afya wa Zambia, alizitaka nchi wanachama kuendeleza hatua za haraka ili kuzuia kuenea kwa mlipuko wa sasa.
Alisema mlipuko huo umeathiri takriban nchi 15 wanachama wa Sadc.
Zambia ni miongoni mwa nchi zinazopambana na mlipuko mbaya zaidi kuwahi kutokea katika miongo kadhaa, huku takriban vifo 600 na visa zaidi ya 16,000 vimeripotiwa tangu Oktoba mwaka jana.
Nchi imekumbwa na milipuko ya kipindupindu angalau mara 30 tangu 1977, huku shirika la kutoa misaada la WaterAid likisema mlipuko wa hivi punde ni mbaya zaidi tangu 2017.
Zimbabwe na Malawi pia zimeathiriwa na mlipuko wa sasa wa kipindupindu.
Viongozi wa Sadc wanatazamiwa kufanya mkutano wa kilele usio wa kawaida siku ya Ijumaa ili kutathmini hali ya kujiandaa na kukabiliana na milipuko ya kipindupindu.
Chanzo: Bbc
-
Uzazi/Ujauzito5 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Magonjwa4 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Uzazi/Ujauzito3 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa7 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Magonjwa2 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events6 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News5 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
Utafiti24 hours ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO