News
TANZIA: Makamu Mwenyekiti wa zamani Simba SC afariki Dunia
TANZIA: Makamu Mwenyekiti wa zamani Simba SC afariki Dunia
Aliyewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa Simba SC miaka ya 1990, Fakhruddin Amijee amefariki dunia jana jioni nyumbani kwake Arusha akiwa ana umri wa miaka 84 baada ya kusumbuliwa na maradhi kwa muda mfupi .
Amijee aliyewahi pia kuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Wavu Dar es Salaam (TAREVA) na Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Kikapu Tanzania (TABA) amezikwa jana hiyo hiyo usiku Jijini Arusha.
Amijee alikuwa Makamu Mwenyekiti Simba kuanzia mwaka 1990 chini Mikidadi Kasanda, Juma Salum baadaye chini ya Ally Amir ‘Bamchawi’ na Priva Mtema (wote marehemu) mwaka 1996 na baada ya hapo akahamia kwenye michezo mingine na kuongoza TAVA na TABA.
Enzi za uhai wake marehemu Amijee alikuwa kiongozi wa msafara wa mechi zote za ugenini Simba wakifika Fainali Kombe la CAF mwaka 1993.
Lakini pia atakumbukwa kwa kuileta klabu ya Stoke City ya England ambayo ilicheza mechi za kirafiki na timu za Simba, Yanga Uwanja wa Taifa, sasa Uhuru Jijini Dar es Salaam na Coastal Unión Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga.
Amijee ameacha mke, Sukaina na watoto watatu, Zahra, Husain na Zainab.
Mungu ampumzishe kwa amani. Amín.
-
Uzazi/Ujauzito6 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Uzazi/Ujauzito4 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa5 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Magonjwa3 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events7 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News5 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
afyatips18 hours ago
Madhara ya damu kuwa nyingi mwilini
-
Utafiti2 days ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO