News
kijana Ramadhan Hassan (18) kutoka Tanga apate matibabu bure ya ugonjwa alionao
kijana Ramadhan Hassan (18) kutoka Tanga apate matibabu bure ya ugonjwa alionao.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameelekeza kijana Ramadhan Hassan (18) kutoka Tanga apate matibabu bure ya ugonjwa alionao katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Rais Samia ametoa maelekezo hayo kufuatia habari iliyorushwa na Globaltvonline ikimuonyesha Ramadhan akihitaji msaada wa matibabu.
Bi. Prisca Manfredi ambaye ni mlezi wa Ramadhani amesema kuwa kijana huyo alisafiri peke yake kutoka Tanga bila ya kuwa na mwangalizi kutokana na ukosefu wa fedha na sasa hupo Mkoa wa Pwani kwa ajili ya matibabu lakini hali imekuwa ngumu kutokana na wao kusosa fedha za matibabu hivyo wanahitaji msaada wa matibabu.
Tunaipongeza Global Tv kwa kuibua habari hii kuhusu kijana huyu mweney uhitaji wa matibabu na sasa Ramadhani Hassan atasafirishwa kuelekea Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya uchunguzi na matibabu bure kwa ugonjwa alionao huku gharama za matibabu yake zitalipwa na Wizara ya Afya.
-
Uzazi/Ujauzito5 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Magonjwa4 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Uzazi/Ujauzito3 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa7 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Magonjwa2 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events6 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News5 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
Utafiti24 hours ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO