Connect with us

News

Mtambo ulivyoua 11 kiwanda cha Mtibwa Morogoro

Avatar photo

Published

on

Mtambo ulivyoua 11 kiwanda cha Mtibwa Morogoro

Baadhi ya wafanyakazi wa Kiwanda cha Sukari cha Mtibwa kilichopo Tuliani, Morogoro wameeleza jinsi bomba linalozalisha mvuke wa joto lilivyolipuka na kusababisha vifo vya wenzao 11 na wengine kujeruhiwa.

Alfajiri leo Mei 23, 2024 wakati wakijiandaa kuanza uzalishaji kiwandani hapo, ndipo bomba hilo linalopokea mvuke wenye joto kali limelipuka na kuwaathiri waliokuwa kwenye chumba cha uendeshaji mitambo.

Meneja wa umeme katika kiwanda hicho, Juma Balanda amesema imetokea hitilafu iliyosababisha bomba hilo kulipuka.

“Ajali imetokea baada ya bomba la kupokea mvuke wa joto ambalo linafikia nyuzijoto 450 kupasuka na lile joto kuwazidi wale watumishi na kufariki dunia.

“Awali tulikuwa na shughuli ya maboresho kwenye mitambo yetu kwenye mfumo wa kusafirisha joto, hivyo kabla ya kuanza uzalishaji rasmi, ndio ukatokea mpasuko ambao umeleta madhara haya.

“Waliofariki ni watu 11, katika hao mmoja ni raia wa Brazil ambaye alikuwa fundi mkuu, mwingine ni raia wa Kenya ambaye ni mtaalamu wa umeme, mwingime ni raia wa India ambaye ndiye alikuwa meneja na wengine wanane ni Watanzania,” amesema.

Amesema chumba kilikuwa na wataalamu na waendeshaji waliofikia 16, mmoja alitoka kwenda chumba kinachochochea joto, yeye alitoka nje kuzungumza na simu na mtumishi mwingine alimkuta nje.

Balanda amesema wakati wako nje, ukatokea mlipuko kwa sauti kubwa, moshi mkubwa ulitanda na vijana wawili wakatoka wakiwa na hali mbaya, kwa kuwa joto lilikuwa kubwa na kilichowasaidia ni kwamba mvuke haukuwapiga moja kwa moja lakini waliungua ngozi ya juu.

“Nilikuwa nimechanganyikiwa lakini baadaye nikawachukua, nikawawahisha hospitali. Wakati narudi kutoka hospitali, nikaona miili ya watu imelala, wote wakiwa wameshafariki dunia,” amesema meneja huyo.

Manusura mwingine wa ajali hiyo ambaye hakutaka kutaja jina lake, ameliambia Mwananchi kuwa yeye aliingia kazini Mei 22, 2024 kuanzia asubuhi hadi saa 3 usiku muda wa kutoka.

“Jana, shifti yangu ilikuwa asubuhi hadi saa 3 usiku, nilipotoka kwenda nyumbani nikapigiwa simu baada ya kumaliza kuoga nirudi kazini, maana kulikuwa na majaribio ya mitambo ili tuanze uzalishaji, nikakubali.

“Nikarejea, nilipofika tukaanza majaribio lakini wakati hatujaruhusu ule mvuke uanze kusambaa kwenye mtambo wake, ndipo bomba likapasuka na mimi nilikuwa chumba cha pili sikupata madhara yoyote, kwa kuwa joto lile linafikia nyuzijoto 450 halikunifikia, basi wale tuliokuwa nao wakafariki baada ya mlipuko huo,” amesema.

Kwa upande wake, fundi mwingine ambaye ni fundi mkuu wa kitengo linapozalishwa joto la kuendesha mtambo huo, ambaye pia hakutaka kutaja jina lake, amesema ni kama bahati kwake kuwa hai.

“Ule mtambo ulikuwa unatengenezwa, tulianza majaribio tangu jana mchana, kila tukijaribu haukubali, sasa tukatengeneza mara ya mwisho kwa ule usiku ili tujaribu kwa mara ya mwisho, tukafunga kila kitu, tukaanza kuzalisha joto ili lifikie 450, kisha tuliruhusu kwenda panapohusika ili tujaribu tuone kama joto na presha vinapanda kwa pamoja.

“Kabla kiwango cha joto tulichotaka hakijafika, ghafla nikasikia mlipuko mkubwa, kumbe kuna bomba lilizidiwa na kupasuka, basi wenzetu wakafariki katika mazingira hayo na mimi nilikuwa upande mwingine,” amesema.

Mganga mfawidhi katika Hospitali ya Turiani, David Ruchwaisa amesema wamepokea majeruhi wawili kutoka kwenye ajali hiyo.

“Tumepokea wagonjwa wawili kutoka kwenye ajali ya kiwanda cha Mtibwa na tumewapa huduma ya kwanza lakini kwa hali zao tunaandaa rufaa ili wasafirishwe kwenda Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dodoma ili wakatibiwe huko.

“Wamepata majeraha sehemu tofautitofaut ikiwemo uso, kifua, tumbo, mgongo, mikono na miguu, hali zao sio nzuri sana, lakini naamini kadri wanavyopata matibabu, afya zao zitaimarika,” amesema.

Katika hospitali ya Kiwanda cha Mtibwa, imeshuhudiwa umati wa watu ambao miongoni mwao ni ndugu wa marehemu waliofika kutambua miili ya ndugu zao, ambapo maofisa wa Jeshi la Polisi waliwasihi wananchi hao kuwa wavumilivu ili uchunguzi ukikamilika wapewe miili kwa ajili ya taratibu wa mazishi.

Wakati huohuo, shughuli kwenye kiwanda hicho zimesimama kwa muda baada ya kutokea kwa hitilafu hiyo na uzalishaji utaanza baada ya uchunguzi wa chanzo cha ajali hiyo kukamilika na taratibu zingine kuhusu ajali hiyo.

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 months ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa3 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa3 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa5 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake5 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa4 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa2 days ago

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri Yapo magonjwa mbali mbali ya ngozi ambayo huweza kuathiri Sehemu za Siri za Mwanaume...

Magonjwa6 days ago

Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu

Dalili za acid reflux: Tatizo la Gastroesophageal reflux disease (GERD), ni tatizo ambalo huwapata Watu wengi,Tatizo hili hujulikana kwa jina...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe au ni ugonjwa ambao huhusisha ngozi kupoteza rangi...

Magonjwa3 weeks ago

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni,...

Magonjwa4 weeks ago

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu Utangulizi: Scabies huhusisha mtu kuwa na vipele na muwasho kwenye ngozi yake ambapo...

Magonjwa4 weeks ago

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume Gono ni neno maarufu ambalo kirefu chake ni Gonorrhea na kiswahili chake ni...

Magonjwa1 month ago

Dalili Mpya za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni Dalili za ukimwi kwenye ngozi Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala...

Magonjwa1 month ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Magonjwa1 month ago

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake Karibu! Hapa kwa makala yenye taarifa muhimu kuhusu...

Magonjwa1 month ago

Vyanzo Vya Kifo cha Ghafla: Sababu Zinazotisha na Jinsi ya Kujikinga

“Vyanzo Vya Kifo cha Ghafla: Sababu Zinazotisha na Jinsi ya Kujikinga” Kifo cha ghafla ni janga lisilotarajiwa ambalo linaweza kumpata...

Trending