Connect with us

News

Plasmolifting: Jinsi wanawake walivyoambukizwa VVU Marekani wakati wa kupodolewa nyuso zao

Avatar photo

Published

on

Plasmolifting: Jinsi wanawake walivyoambukizwa VVU Marekani wakati wa kupodolewa nyuso zao

Maelezo ya picha,Inaaminika kuwa hiki ndio kisa cha kwanza nchini Marekani kutokea wakati wagonjwa waliambukizwa VVU wakati wa kutumia vipodozi.

Habari za hivi punde kwamba wanawake nchini Marekani walipata virusi vya Ukimwi (VVU) wakati wa utaratibu wa kuinua maji ya damu au plasma zilizua maswali kuhusu usalama wa baadhi ya taratibu za urembo.

Kulingana na ripoti ya Taasisi ya Marekani ya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (CDC), angalau wanawake watatu waliambukizwa kwenye saluni ya urembo(spa) huko New Mexico mnamo 2018. Ripoti hiyo pia inasema kuwa visa hivi vinatoa mwanga juu ya njia mpya za kueneza maambukizi.

Hii inaaminika kuwa haya ni maambukizi ya VVU ya kwanza kabisa yanayohusiana na utaratibu wa urembo yaliyoyorekodiwa nchini Marekani.

Je, kuinua plasma ni nini na jinsi gani wanawake waliambukizwa VVU wakati wa utendaji wake? Watu wanaweza kufanya nini ili kujilinda kutokana na maambukizi wakati wa taratibu za vipodozi?

Tunaelezea kile kinachojulikana kuhusu hilo na kile wataalam wanachosema.

Kuinua plasma ni nini

Plasmolifting, au PRP (Platelet Rich Plasma) ni utaratibu wa kawaida wa vipodozi, wakati ambapo mgonjwa hudungwa maji ya damu (plasma) yenye damu yake mwenyewe. Kwa kuwa utaratibu unahusisha vitendo na damu, wakati mwingine huitwa “Dracula therapy”.

Wakati wa utaratibu huu , daktari huchukua damu kutoka kwa mshipa wa mtu, hutumia kifaa maalum kinachotumiwa kutenganisha vimiminika vya mwili (centrifuge) ili kutoa maji ya damu kutoka humo, na kisha kuiingiza chini ya ngozi kwa kutumia sindano nyembamba.

Inaaminika kuwa utaratibu huo unaboresha michakato ya kuzaliwa upya (rejuvenation) kwa ngozi, na kuchochea uzalishaji wa collagen mpya na uwezo wa ngozi kutanuka. Inaweza kupunguza kuonekana kwa makunyanzi au makovu ya upele wa mwili.

Utaratibu huo umejulikana kwa miaka mingi. Nyuma mnamo 2013, nyota wa filamu za maisha halisi Kim Kardashian alionyesha uso wake baada ya kufanyiwa utaratibu huo kwenye Instagram.

Hata hivyo, miaka michache baadaye, Kardashian alisema kwamba hatafanya tena utaratibu huu kwa sababu ulikua “mgumu na ulionisababishia maumivu.”makali.

Utaratibu kawaida huchukua dakika 40.

Jinsi gani wanawake wa New Mexico walipata VVU?

Katika majira ya joto ya 2018, Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa nchini Marekani kilifahamu kuhusu mwanamke wa Marekani mwenye umri wa miaka kati ya 40-50 ambaye alipimwa na VVU akiwa nje ya nchi.

Mwanamke huyo aliripoti kwamba hakutumia dawa za sindano, hakutiwa damu kwenye mishipa hivi majuzi, na hakuwa na mahusiano ya kingono na mtu mwingine yeyote isipokuwa mpenzi wake wa sasa.

Lakini alifichua kuwa alifanyiwa utaratibu wa kuinua uso kwa njia ya kuongezewa plasma kwenye kituo kimoja cha mapodozi huko New Mexico mapema mwaka huo.

Uchunguzi wa CDC uligundua kuwa kituo hicho (spa), ambayo pia ilitoa huduma zingine za sindano kama sindano za Botox (kuongeza makalio) haikuwa na leseni na ilitumia “taratibu zisizo salama za kudhibiti maambukizi.”

Katika jumba hilo, walipata “mirija ya damu isiyo na lebo na sindano za matibabu” zilizohifadhiwa kwenye jokofu la jikoni karibu na chakula, pamoja na “sindano zisizofunikwa” zilizotawanyika ndani ya kabati na kwenye kwenye meza ya mapokezi.

Baadhi ya bakuli za damu pia zilionyesha dalili za kutumika tena, na CDC ilipata angalau mteja mmoja ambaye alipimwa na kuambukizwa VVU kabla ya kutembelea kituo cha matibabu.

Tangu wakati huo, shirika hilo la afya limehusisha kituo hicho na visa vitano vya maambukizi ya VVU, wakiwemo wanawake wanne ambao walifanyiwa taratibu za kuinua nyuso zao kwa kutumia maji ya damu kati ya miezi ya Mei na Septemba mwaka 2018, pamoja na mwanamume ambaye alikuwa katika uhusiano na mmoja wa wanawake hao.

Kulingana na CDC, kwa mwanamume na mwanamke katika uhusiano walioonekana kuwa na maambukizi ya VVU ya hatua ya mwisho walikuwa walipata maambukizi hayo kabla ya kufanyiwa utaratibu huo wa uso.

Kituo hicho cha urembo (Spa) kilifungwa mwishoni mwa 2018, na mmiliki wake wa zamani, Maria de Lourdes Ramos De Ruiz mwenye umri wa miaka 62, anatumikia kifungo cha miaka mitatu na nusu jela. Mnamo 2022, alikiri kufanya utaratibu hu owa matibabu ya urembo bila leseni.

Je, taratibu hizi ni salama?

Mamia ya nyaraka na tafiti za matibabu zilizochapishwa zinaonyesha kuwa kuinua plasma ni bora katika kutibu majeraha ya michezo, chunusi, eczema na hali nyingine za ngozi.

Chama cha Chuo cha Marekani cha tiba ya ngozi kinasema utaratibu yenyewe, ikiwa unafanywa kwa usahihi, ni salama.

“Baadaye, unaweza kupata maumivu kwenye eneo ulipochomwa sindano, pamoja na michubuko kidogo na uvimbe,” shirika linasema athari “Hizi kawaida hupotea ndani ya siku chache.”

Hatari kubwa zaidi inahusiana na jinsi damu inavyochakatwa na kituo kinachotoa matibabu.

“Ni muhimu kwamba damu iliyochukuliwa kutoka kwa mwili wako ni salama. Vinginevyo, unaweza kupata maambukizi,” chama kinasema.

Pia ni muhimu kuhakikisha kwamba damu iliyorudishwa ni ya mteja na si ya mtu mwingine, vinginevyo mpokeaji anaweza kuwa mgonjwa sana.

Wataalamu wanasema kwamba wale wanaotaka kupata matibabu ya urembo wanapaswa kuhakikisha mapema kwamba saluni ina leseni. Pia wanapaswa kuzingatia jinsi wafanyakazi wanavyoshughulikia vifaa vya matibabu kama vile sindano.

Kuinua plasma sio matibabu pekee ya vipodozi ambayo hivi karibuni yamefanya ambayo yamego nga vichwa vya habari kuhusiana na kusababisha magonjwa mabaya.

Maafisa wa afya wa Marekani walionya wiki iliyopita juu ya mlipuko wa ugonjwa wa botulism unaohusishwa na uongezaji gushi wa makalio ambao umepelekea watu 22 kuugua katika majimbo 11, ambao baadhi yao bado wamelazwa hospitalini.

Botulism ni ugonjwa mbaya ambao husababisha kupungua kwa uwezo wa kuona, ugumu wa kumeza na kupumua, na kushindwa kuongea na uchovu.

Sindano za Botox ni utaratibu maarufu unaotumiwa kulainisha mikunjo na kufanya ngozi ionekane changa. Sindano kawaida hugharimu takriban $530 kwa matibabu.

Kama ilivyo kwa kuinua maji ya damu (plasma), CDC inawashauri wale wanaopenda kufanyiwa tiba ya sindano za Botox kutafiti mtoa huduma kabla na kuhakikisha kuwa Botox ambayo mtaalamu wa urembo anaitumia imeidhinishwa na kununuliwa kutoka kwa chanzo kinachotegemewa.

Via:BBC

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 months ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa3 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa3 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa5 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake5 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa4 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu

Dalili za infection kwenye damu Mchafuko wa damu,chanzo,dalili na Tiba Mchafuko wa damu; hiki ni kiswahili ambacho watu wamezoea kukitumia...

Magonjwa4 days ago

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri Yapo magonjwa mbali mbali ya ngozi ambayo huweza kuathiri Sehemu za Siri za Mwanaume...

Magonjwa1 week ago

Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu

Dalili za acid reflux: Tatizo la Gastroesophageal reflux disease (GERD), ni tatizo ambalo huwapata Watu wengi,Tatizo hili hujulikana kwa jina...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe au ni ugonjwa ambao huhusisha ngozi kupoteza rangi...

Magonjwa4 weeks ago

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni,...

Magonjwa4 weeks ago

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu Utangulizi: Scabies huhusisha mtu kuwa na vipele na muwasho kwenye ngozi yake ambapo...

Magonjwa1 month ago

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume Gono ni neno maarufu ambalo kirefu chake ni Gonorrhea na kiswahili chake ni...

Magonjwa1 month ago

Dalili Mpya za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni Dalili za ukimwi kwenye ngozi Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala...

Magonjwa1 month ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Magonjwa1 month ago

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake Karibu! Hapa kwa makala yenye taarifa muhimu kuhusu...

Trending