Magonjwa
Ugonjwa wa Gambiense Sleeping Sickness,African Trypanosomiasis
![](https://afyaclass.com/mk_omb/uploads/2022/11/200px-PMC5373517_pntd.0005324.g001.png)
Ugonjwa wa Gambiense Sleeping Sickness,African Trypanosomiasis,chanzo,dalili na Tiba yake
Ugonjwa huu hujulikana kama African Trypanosomiasis au kwa Jina lingine “sleeping sickness”
Jina la African Trypanosomiasis ni kwa sababu ya Ugonjwa huu kuwepo Afrika Hasa sub-Saharan Africa,
CHANZO CHA UGONJWA HUU NI NINI?
Ugonjwa huu husababishwa na parasites wadogo sana kutoka kwenye jamii ya Trypanosoma brucei,
Kisha kusambazwa na tsetse fly (Glossina species),
Wanyama wa kufugwa na wanyama wa msituni huweza kuhifadhi Parasite hawa, wanyama hao ni kama Nguruwe, Mbwa,mbuzi, n.k
Na pia Binadamu anaweza kuwa Main reservoir wa Infection hii.
Kuna Species mbili za Trypanosoma brucei;
(1)Trypanosoma brucei-gambiense
(2) Trypanosoma brucei-rhodesiense
T. b. gambiense wanasababisha African trypanosomiasis hasa kwenye eneo la western na central Africa wakati T. b. rhodesiense husababisha African trypanosomiasis hasa hasa kwenye eneo la eastern na southern Africa.
DALILI ZA UGONJWA HUU WA SLEEPING SICKNESS
Ugonjwa huu umepewa jina la Sleeping sickness kwa Sababu Dalili zake huweza kujumuisha matatizo ya Usingizi,
– Baada ya Mtu kung’atwa na tsetse fly anaweza kupata maumivu kisha kuwa na kidonda chekundu(red sore) ambacho huitwa chancre.
– Mtu kupata homa
– Mtu kupata maumivu makali ya Kichwa
– Mwili kutokutulia(irritability)
– Mtu kupata uchovu usio wa kawaida
– Mara nyingi Mtu wenye Ugonjwa huu wa Sleeping sickness hupata maumivu ya Misuli Pamoja na Joints
– Baadhi ya watu hupata vipele kwenye ngozi au Skin rashes
– Mtu kuwa kama amechanganyikiwa
– Wagonjwa wachache huweza Kuvimba Uso
– Na kama mgonjwa hajapata Tiba maambukizi haya huweza kuwa makali zaidi na kusababisha Kifo
MATIBABU YA UGONJWA HUU WA SLEEPING SICKNESS
Matibabu ya Ugonjwa huu hutegemea na aina ya maambukizi(T. b. gambiense au T. b. rhodesiense) pamoja na hatua ya Ugonjwa ulipofikia.
Dawa kama Pentamidine,suramin, melarsoprol, eflornithine, nifurtimox huweza kutumika.
-
Uzazi/Ujauzito6 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Uzazi/Ujauzito4 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa5 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Magonjwa3 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events7 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News5 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
afyatips18 hours ago
Madhara ya damu kuwa nyingi mwilini
-
Utafiti2 days ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO