News
Baba amuua mtoto wake wa miezi 6 kwa kumpiga hadi kufa
Baba amuua mtoto wake wa miezi 6 kwa kumpiga hadi kufa.
Baba mmoja mwenye umri wa miaka 29 kutoka nchini Uingereza amepatikana na hatia ya kumuua mtoto wake wa kiume mwenye umri wa miezi sita ambaye waendesha mashtaka walisema ‘alitikiswa na kupigwa’ kabla ya kufa.
David Hollick, 29, alikanusha mauaji na shtaka lingine la kuua bila kukusudia kuhusiana na kifo cha mwanawe mchanga Kairo Jax Hollick, aliyefariki katika Hospitali ya Birmingham Children’s Hospital tarehe 12 Februari 2020, siku chache baada ya kupata jeraha la ubongo lisiloweza kupona.
Mahakama ya wanawake 10 na wanaume wawili ilichukua karibu saa 20 kupata majibu kuwa Hollick, wa Primley Avenue, Walsall, hana hatia ya mauaji lakini ana hatia ya kuua bila kukusudia,Jumatatu alasiri.
Katika Kesi hiyo,inasemekana kwamba pamoja na jeraha la ubongo, Kairo alikuwa amevunjika fuvu la kichwa mara mbili na kuvunjika mkono wake wa kulia alipokuwa chini ya uangalizi wa babake mnamo Februari 9.
Mwendesha mashtaka David Mason KC aliambia mahakama kwamba Kairo ‘hakutikiswa tu kwa nguvu, lakini pia kichwa chake kilikuwa kimepigwa angalau mara mbili’ kwa kitu kigumu na Hollick.
Mpenzi wa zamani wa Hollick Adina Johnson alikuwa amemuacha mtoto wao nyumbani kwake kama kawaida mnamo Februari 7 wikendi na Kairo hakuwa na tatizo lolote wakati huo, na yeye hakuwa na wasiwasi wowote kuhusu afya yake.
Hollick alikuwa akikaa katika chumba cha kuhifadhia Vitu katika nyumba ya wazazi wake kwa sababu ya ukosefu wa chumba cha kulala baada ya kurejea kwao wakati uhusiano wake na Bi Johnson ulipoisha.
Mnamo saa 4:30 asubuhi, Hollick aliingia katika chumba cha kulala cha baba yake katika kile waendesha mashtaka walisema ‘hali ya hofu’, wakisema kwamba Kairo alikuwa hapumui na kwamba ‘hakutaka kumpoteza’.
Kairo alikimbizwa katika Hospitali ya Walsall Manor, ambapo Hollick aliwaambia wahudumu wa afya kuwa alimsikia mtoto wake akilia kabla hajaacha kupumua na kudai alimtikisa tu ili ‘kumuamsha’.
-
Uzazi/Ujauzito6 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Uzazi/Ujauzito4 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa5 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Magonjwa3 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events7 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News5 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
afyatips18 hours ago
Madhara ya damu kuwa nyingi mwilini
-
Utafiti2 days ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO