Magonjwa
DALILI ZA UTI KWA WOTE(MWANAMKE NA MWANAUME)
![](https://afyaclass.com/mk_omb/uploads/2022/06/images-5-1.jpeg)
DALILI ZA UTI KWA WOTE(MWANAMKE NA MWANAUME)
Katika makala hii,nmekupa baadhi ya dalili ambazo ukiziona zinatokea kwenye mwili wako,
unaweza kuwa na maambukizi ya kwenye njia ya Mkojo au UTI
KUMBUKA; UTI ni kifupi cha maneno haya “Urinary tract Infection”
Hapa tunazungumzia maambukizi ya vimelea vya magonjwa kama vile bacteria,
ambayo huhusisha mfumo wa mkojo ikiwemo;Njia ya mkojo,kibofu cha mkojo,Figo N.k
Unaweza kupata maambukizi ya bacteria kwenye Njia ya Mkojo(UTI) ambayo hujirudia mara kwa mara yaani recurrent infections,
Tatizo la UTI Sugu,UTI ambayo haiishi au UTI ambayo hujirudia rudia mara kwa mara huweza kusababisha madhara zaidi,ikiwemo;
- Kusababisha tatizo la Uke kuwa Mkavu zaidi kwa Mwanamke
- Kuathiri mzunguko wa hedhi
- Kupelekea matatizo mengine kama PID,wakati bacteria wakipenya na kuingia kwenye via vya uzazi vya mwanamke n.k
DALILI ZA UTI KWA WOTE(MWANAMKE NA MWANAUME) NI PAMOJA NA;
-Kupata maumivu makali ya nyonga,
– Kupata maumivu ya mgongo,
– Kupata maumivu ya joint pamoja na viungo mbali mbali vya mwili
– Kupata maumivu ya tumbo hasa hasa upande wa kushoto
– Kuhisi kukojoa mara kwa mara ila ukikojoa mkojo haushi
– Kuhisi hali ya kuchoma wakati wa kukojoa
– Kukojoa mkojo wenye rangi kama pink au nyekundu,hii ni baada ya UTI kuwa ya mda mrefu na kuanza kuleta madhara makubwa
– Kuhisi hali ya uume kuwaka Moto
– Kuhisi hali ya kuchoma au kuwasha kwenye tundu au njia ya mkojo
– Kupata uchovu wa mwili kupita kiasi au Mwili kuchoka sana
– Joto la mwili kuwa juu au Mtu kuwa na Homa(Fever)N.k
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.
-
Magonjwa4 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Elimu&Ushauri6 days ago
Afya za watu bilioni 1.8 duniani matatani kwa kutokufanya Mazoezi – WHO
-
Uzazi/Ujauzito2 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Magonjwa1 day ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Events3 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News6 days ago
Mlipuko Mbaya wa homa ya nyani watokea tena KIVU KASKAZINI
-
Uzazi/Ujauzito10 hours ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
News2 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani