Magonjwa
Dalili za fangasi sehemu za siri(Wananawake na Wanaume)
Dalili za fangasi sehemu za siri(Wananawake na Wanaume)
Candida Albicans ni jamii ya fangasi ambao hupenda sana kushambulia maeneo ya sehemu za siri, fangasi hawa hushambulia wanawanake na wanaume pia, Ingawa aina hii ya Fangasi hupenda kushambulia sehemu za siri za Mwanamke zaidi ya Mwanaume.
DALILI ZA FANGASI SEHEMU ZA SIRI
(A). KWA MWANAUME
1. Kupata miwasho sehemu za siri,Kuzunguka eneo la uume,pamoja na ngozi yote ya korodani na eneo la chini linalotenganisha kati ya Njia ya haja kubwa na Uume, na wakati mwingine miwasho hufika mpaka eneo la haja kubwa
2. Kupata hali ya ngozi kuvimba ambayo hii hupendelea sana kutokea maeneo ya karbu na njia ya haja kubwa
3. Ngozi ya korodani kubadilika rangi na kuwa nyekundu mithili ya mtu aliyeunguzwa
4. Ngozi ya eneo la uume hasa hasa chini ya uume karibu na korodani kubadilika rangi na kuwa nyekundu
5. Kupata michubuko sehemu za siri
6. Na wakati mwingine mwanaume kuhisi maumivu wakati wa kufanya mapenzi
7. Kuhisi kama hali ya kuungua kwenye ngozi ya eneo la sehemu za siri
8. Kutoa harufu mbaya sehemu za siri japo dalili hii huwatokea sana wanawake
(B). KWA MWANAMKE
– Kupatwa na miwasho sehemu za Siri au kuwashwa ukeni
– Kutokwa na uchafu wenye harufu mbaya pamoja na rangi kama Maziwa ya Mgando
– Ngozi inayozunguka sehemu za siri au ngozi ya mashavu ya uke kuwa nyekundu
– Kupatwa na vidonda pamoja na michubuko sehemu za Siri
– N.K
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.
-
Uzazi/Ujauzito5 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Magonjwa4 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Uzazi/Ujauzito3 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa7 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Magonjwa2 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events6 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News4 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
Utafiti21 hours ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO