News
Misri kuwezesha uhamisho wa watu 7,000 wa kigeni kutoka Gaza
Misri kuwezesha uhamisho wa watu 7,000 wa kigeni kutoka Gaza
Misri inataka kuwezesha uhamisho wa wageni 7,000 walio na uraia kutoka nchi 60 huko Gaza kupitia kivuko cha ardhini cha Rafah.
Hatua hiyo ilijadiliwa wakati wa mkutano uliofanyika na maafisa wa Misri na mabalozi na wawakilishi wa nchi za nje jana, Jumatano.
Mamlaka ya Palestina ilichapisha orodha ya pili ya majina ya takribani raia 600 wa kigeni, wakiwemo raia 400 wa Marekani, ambao wataruhusiwa kuvuka kuingia Misri kuanzia leo.
Misri pia ilijadili maandalizi ya kupokea Wapalestina waliojeruhiwa na juhudi za Misri kuleta msaada.
Misri ilipokea Wapalestina 46 waliojeruhiwa kati ya 81, ambao walihamishiwa katika hospitali za Sheikh Zuweid, Al-Arish, na Bir Al-Abd.
Kivuko cha Rafah kilifunguliwa jana, Jumatano, kwa idadi ndogo ya majeruhi, wageni, na wenye hati za kusafiria za kigeni kuvuka, kwa mara ya kwanza tangu kuanza kwa vita.
Chanzo:Bbc
-
Uzazi/Ujauzito5 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Magonjwa4 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Uzazi/Ujauzito3 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa7 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Magonjwa2 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events6 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News4 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
Utafiti21 hours ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO