Connect with us

News

Fahamu aina ya mbwa rafiki kufugwa na hatua za kufuata kabla na wakati wa kuwafuga viumbe hawa

Avatar photo

Published

on

Fahamu aina ya mbwa rafiki kufugwa na hatua za kufuata kabla na wakati wa kuwafuga viumbe hawa.

Mwanza. Wataalamu wametaja sababu za mbwa kumshambulia mmiliki wake au watu wanaomzunguka, wakieleza njia za kuepuka hatari hiyo.

Hayo yanaelezwa zikiwa zimepita siku nne tangu kusambaa taarifa ya mama na watoto wawili, wakazi wa Usagara wilayani Misungwi mkoani Mwanza, kunusurika kifo baada ya kushambuliwa na mbwa waliokuwa wakimfuga.

Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Januari 8, 2024.

Baba wa familia hiyo, Nicholas Kunju alisema walifuga mbwa wawili, wa jike (pitbull) na  dume (bulldog) kwa takribani miaka saba.

Swali analojiuliza ni nini kilitokea hadi mbwa dume akachachamaa na kuwashambulia watoto na mke wake?

Akijiuliza hayo, kwenye mitandao ya kijamii waliofuatilia habari hiyo waliibua maswali, Je? ni aina gani ya mbwa ni rafiki kufugwa na hatua za kufuata kabla na wakati wa kuwafuga viumbe hao.

Akizungumza na Mwananchi Digital, mtaalamu wa mifugo, Joseph Ndalu amesema sababu za mbwa kuwashambulia wamiliki wake zinatofautiana kulingana na mazingira.

Amesema utamaduni wa kufuga wanyama hao kiholela na kwa mazoea ni sababu kuu.

Ndalu ametaja sababu nyingine kuwa ugonjwa wa kichaa cha mbwa, kutopewa chanjo na dawa za kuua vimelea wa nje na ndani, ikiwamo minyoo, kutopewa chakula kwa wakati na ujazo unaohitajika, kufanyishwa michezo wasiyoipenda na kuanzisha mazingira hatarishi kwa kiumbe huyo.

“Tunasisitiza wananchi kuwatumia maofisa mifugo waliopo kwenye kila kata ili kupata uelewa wa aina ya mbwa wa kufuga kulingana na mahitaji,” amesema Ndalu.

Aina za mbwa

Ndalu amesema mbwa wamegawanyika katika makundi makuu mawili ambayo ni wenye maumbile makubwa na madogo.

Kundi la wenye maumbile makubwa, amesema ndilo hatarishi, linalohitaji umakini mkubwa na tahadhari. Linaundwa na mbwa aina ya Bulldog, Pitbull, Rottweiler na Cane corso.

“Kundi linaloundwa na ‘bulldog’ halihitaji msongo wa mawazo unaochangiwa na kutopewa chakula, matibabu au chanjo kwa wakati. Usipotimiza wajibu huo wana tabia ya kuchukia, hata ukimfungulia anaweza kukushambulia na wakati mwingine ukimkataza hawezi kutii amri,” anasema na kuongeza:

“Ndiyo maana matukio mengi ya watu kushambuliwa na mbwa duniani, ukifuatilia kwa kiasi kikubwa wanaoshambulia ni mbwa jamii ya ‘bulldog’ ambao wanahitaji kutimiziwa mahitaji yao kwa wakati na usahihi.”

Ndalu amewataka wamiliki au waangalizi wa mbwa hao kuhakikisha wanajenga uzio imara ili wasiruke na kuchangamana na kelele za nje.

Anashauri wafunguliwe kuanzia saa nne usiku hadi saa 12 asubuhi akieleza muda huo hauna msongamano mkubwa wa watu.

Kuhusu mbwa wenye maumbile madogo (ya kawaida), Ndalu amesema linaundwa na German Sherpherd, Golden Retriever (Scottish) na Belgian Sherpherd, Maltese (wa urembo), Basenji, Kuvinda na wa kawaida (local breed).

“Hawa ni mbwa ambao hawahitaji uangalizi wa hali ya juu hata kama ikitokea changamoto si rahisi kumgeuka mmiliki wake na kumshambulia. Hiyo jamii ya Sherpherd, Basenji na Kuvinda ni mbwa wasikivu na hutumika kwenye ulinzi na uwindaji, pia wanafundishika kwa urahisi,” amesema Ndalu.

Ili kuepuka madhara, mtaalamu huyo ameishauri jamii kufuata kanuni na utaratibu wa ufugaji wanyama kwa kupewa ushauri wa aina ya mbwa na matumizi yake.

Amesema kutofuata utaratibu kunaweza kuleta madhara ikiwemo kusambuliwa na wanyama hao.

Kwa upande wake, Charles Oging’, mtaalamu wa mifugo amesema japokuwa ‘bulldog’ si wakali na wakorofi kulinganisha ‘Rottweiler’ kuna mazingira manne yanayoweza kusababisha wabadilike tabia na hata kuwashambulia wamiliki, watu wanaowatunza na wageni bila kutarajiwa.

“Moja ya sababu zinazoweza kumfanya mbwa kumshambulia mtu yeyote ni ugeni, lakini dume pia wanaweza kubadilika tabia na kumshambulia mtu yeyote anayemsogelea mbwa jike aliye kwenye heat (nyakati za kutunga mimba) kwa sababu ya tabia ya wivu,” amesema.

Mtaalamu huyo amesema maradhi yakiwamo kichaa cha mbwa yanaweza kusababisha mnyama huyo kumshambulia mmiliki, anayemtunza au wageni.

Tukio la Usagara

Nicholas Kunju, mkazi wa Usagara wilayani Misungwi mkoani Mwanza, ambaye familia yake ilijeruhiwa kwa kushambuliwa na mbwa aina ya ‘bulldog’ amesema alikuwa dume aliyekuwa akimfuga.

“Familia huwa tunaishi naye pamoja na mtu wa kuwatunza, watoto wangu walirejea likizo kutoka shule, sasa zile movement ‘kutembea’ kwa watoto ndani wale mbwa walihisi upendo umepungua kwao,” alisema Kunju.

Amesema mbwa huyo hakuonyesha dalili za kichaa wala hasira.

“Mtoto mmoja ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha nne alitoka usiku kufanya shughuli zake nje, yule mbwa dume akamnyemelea na kumtishia, kisha akamshambulia kaka yake,” amesema.

Kunju amesema, “mama watoto wangu aliposikia kelele naye akatoka nje na kuanza kusaidiana na mbwa jike kumdhibiti dume, baadaye wakafanikiwa kuingia ndani na kufunga mlango.”

“Ikabaki fujo nje kwa sababu mbwa wote walibaki wakibweka, ndipo majirani waliposikia na kupiga simu polisi, askari walifika na kuwapiga risasi wakafa ndipo tukaingia ndani kuwapatia msaada wa kuwapeleka hospitali,” amesema Kunju.

Amesema baada ya kupatiwa huduma ya kwanza ya kuchomwa sindano ya kichaa cha mbwa katika Hospitali ya CF, aliipeleka familia yake katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando kwa vipimo vya maambukizi ya vimelea.

“Bugando wamewapima damu kuangalia iwapo kuna maambukizi ya vimelea, tofauti na zile dawa walizochomwa za kichaa cha mbwa, wamepatiwa dawa ya kuchoma kukomesha vimelea hivyo,” amesema.

Karibu AfyaUpdates Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In https://afyaclass.com  Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 months ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa3 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa3 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa5 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake5 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa4 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu

Dalili za infection kwenye damu Mchafuko wa damu,chanzo,dalili na Tiba Mchafuko wa damu; hiki ni kiswahili ambacho watu wamezoea kukitumia...

Magonjwa4 days ago

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri Yapo magonjwa mbali mbali ya ngozi ambayo huweza kuathiri Sehemu za Siri za Mwanaume...

Magonjwa1 week ago

Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu

Dalili za acid reflux: Tatizo la Gastroesophageal reflux disease (GERD), ni tatizo ambalo huwapata Watu wengi,Tatizo hili hujulikana kwa jina...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe au ni ugonjwa ambao huhusisha ngozi kupoteza rangi...

Magonjwa4 weeks ago

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni,...

Magonjwa4 weeks ago

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu Utangulizi: Scabies huhusisha mtu kuwa na vipele na muwasho kwenye ngozi yake ambapo...

Magonjwa1 month ago

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume Gono ni neno maarufu ambalo kirefu chake ni Gonorrhea na kiswahili chake ni...

Magonjwa1 month ago

Dalili Mpya za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni Dalili za ukimwi kwenye ngozi Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala...

Magonjwa1 month ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Magonjwa1 month ago

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake Karibu! Hapa kwa makala yenye taarifa muhimu kuhusu...

Trending