News
Mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu kwa mara ya pili watokea SIMIYU
![](https://afyaclass.com/mk_omb/uploads/2024/03/images-8.jpeg)
Mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu kwa mara ya pili watokea SIMIYU
SIMIYU; Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Dk Yahaya Nawanda, amepiga marufuku watu kula kwenye misiba, kutokana na kuibuka tena kwa ugonjwa wa kipindupindu katika Wilaya za Meatu, Bariadi na Itilima.
Hiyo ni mara ya pili kwa mkoa huo kukumbwa na mlipuko wa ugonjwa huo, ambapo mara ya kwanza ilikuwa Desemba, 2023 hadi Januari, 2024 na kusababisha uwepo wa wagonjwa 273 huku vifo vikiwa vitatu.
Akizungumza na viongozi mbalimbali wa mkoa huo, Dk Nawanda ameagiza kuanza kutekelezwa kwa mara nyingine marufuku ya watu kula misibani, kwani katika awamu ya pili ya mlipuko wa ugonjwa huo chanzo kikubwa imeonekana kuwa ni misiba.
“ Awamu ya kwanza tulipiga marufuku na tukafanikiwa kudhibiti ugonjwa huu, sasa umerudi tena, naagiza hapa tunasitisha tena watu kupika na kula misibani, imeonekana misiba imekuwa chanzo kikubwa cha ugonjwa huu,” amesema Dk Nawanda n kuongeza:
“ Tukimaliza kuzika kila mtu nyumbani, hakuna kupika wala kula kwenye misiba, awamu hii ya pili ugonjwa umekuja kwa kasi hasa Wilaya ya Meatu, na wote walipatwa na ugonjwa huu wameutoa misibani baada ya kula chakula.”
Mganga Mkuu wa Mkoa Dk Boniphace Marwa, amesema kuwa mlipuko wa awamu ya kwanza mkoa ulifanikiwa kuudhibiti, ambapo uwepo wa marufuku ya kula misibani na kufungwa kwa minada ilisaidia kwa kiasi kikubwa.
• Soma Zaidi hapa; kuhusu ugonjwa wa kipindupindu,chanzo,dalili na Tiba
-
Magonjwa6 days ago
Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu
-
magonjwa ya wanawake5 days ago
Dalili za Ectopic pregnancy,Mimba kutunga nje ya kizazi
-
Elimu&Ushauri4 days ago
Afya za watu bilioni 1.8 duniani matatani kwa kutokufanya Mazoezi – WHO
-
Magonjwa2 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Events1 day ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News4 days ago
Mlipuko Mbaya wa homa ya nyani watokea tena KIVU KASKAZINI
-
Events6 days ago
Princess Anne alilazwa hospitalini na majeraha madogo kufuatia tukio nyumbani kwake
-
Uzazi/Ujauzito10 hours ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji