News
Ndege mbili zagongana angani jijini Nairobi
![](https://afyaclass.com/mk_omb/uploads/2024/03/Screenshot_20240305-173441.png)
Ndege mbili zagongana angani jijini Nairobi.
Mamlaka ya usafiri wa anga nchini Kenya KCAA imethibitisha katika taarifa kwenye mtandao wa X kuwa ndege aina ya Dash 8 kutoka kampuni ya Safarilink imegongana angani na ndege ndogo ya wanafunzi aina ya Cessna 172 mwendo wa saa tatu na robo asubuhi.
Hakuna maelezo kamili juu ya majeruhi au vifo vyovyote kutoka kwa vyombo husika.
Ndege ya Safarilink ilikuwa safarini kuelekea Diani, pwani ya Kenya ikiwa na abiria 39 na wahudumu watano huku ndege ya mafunzo ya Cessna 172 inamilikiwa na chuo cha mafunzo ya urubani ya Ninety-Nines.
Mamlaka ya KCAA imesema kuwa uchunguzi umeanzishwa unaohusisha vyombo mbali mbali husika, ukiongozwa na idara ya ajali za ndege nchini Kenya AAID, kujua chanzo cha ajali hiyo.
-
Magonjwa4 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Elimu&Ushauri6 days ago
Afya za watu bilioni 1.8 duniani matatani kwa kutokufanya Mazoezi – WHO
-
Uzazi/Ujauzito2 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Magonjwa1 day ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Events3 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
Uzazi/Ujauzito10 hours ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
News6 days ago
Mlipuko Mbaya wa homa ya nyani watokea tena KIVU KASKAZINI
-
News2 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani