News
Ndege mbili zagongana angani jijini Nairobi
Ndege mbili zagongana angani jijini Nairobi.
Mamlaka ya usafiri wa anga nchini Kenya KCAA imethibitisha katika taarifa kwenye mtandao wa X kuwa ndege aina ya Dash 8 kutoka kampuni ya Safarilink imegongana angani na ndege ndogo ya wanafunzi aina ya Cessna 172 mwendo wa saa tatu na robo asubuhi.
Hakuna maelezo kamili juu ya majeruhi au vifo vyovyote kutoka kwa vyombo husika.
Ndege ya Safarilink ilikuwa safarini kuelekea Diani, pwani ya Kenya ikiwa na abiria 39 na wahudumu watano huku ndege ya mafunzo ya Cessna 172 inamilikiwa na chuo cha mafunzo ya urubani ya Ninety-Nines.
Mamlaka ya KCAA imesema kuwa uchunguzi umeanzishwa unaohusisha vyombo mbali mbali husika, ukiongozwa na idara ya ajali za ndege nchini Kenya AAID, kujua chanzo cha ajali hiyo.
-
Uzazi/Ujauzito5 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Magonjwa4 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Uzazi/Ujauzito3 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa7 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Magonjwa2 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events6 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News4 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
Utafiti21 hours ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO