News
Baba wawili ndugu,mmoja mwisraeli na mwingine Mpalestina wakutana baada ya binti zao wawili kufia Vitani
Bassam Aramin, Mwislamu wa Kipalestina, na Rami Elhanan, Myahudi wa Kiisraeli, walipoteza binti zao wachanga katika vita vya Mashariki ya Kati.
Wote wawili wanaishi Israeli, ambako watu wengi wangetarajia wawe kama maadui baada ya msiba huo.
Lakini badala ya kulipiza kisasi, Bassam na Rami walichagua njia tofauti: amani na urafiki.
Polisi wa Israel alimpiga risasi binti wa Bassam, Abir, na kumjeruhi vibaya akiwa na umri wa miaka 10. Binti ya Rami, Smadar, aliuawa katika shambulio la kujitoa mhanga la Hamas, akiwa na umri wa miaka 14.
Wanasema “maumivu yasiyovumilika” yamewafanya wajenge urafiki usioweza kutenganishwa kati ya “ndugu” – jinsi wanavyoita uhusiano wao.
CHANZO CHA PICHA,BASSAM ARAMIN / RAMI ELHANAN
Binti ya Bassam, Abir (kushoto) alikuwa na umri wa miaka 10 alipouawa, na binti ya Rami, Smadar (kulia), alikuwa na umri wa miaka 14 alipouawa.
“Sisi si wanyama, na tunaweza kutumia akili zetu. Na unaanza kujiuliza maswali kama haya – je, kuua mtu yeyote kutamrudisha binti yangu?” Rami alihoji.
“Hata kama utaua Wayahudi wengine wote duniani – sio tu Waisraeli – hautawahi kukutana na binti yangu tena,” alisema Bassam.
-
Uzazi/Ujauzito6 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Uzazi/Ujauzito4 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa5 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Magonjwa3 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events7 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News5 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
afyatips18 hours ago
Madhara ya damu kuwa nyingi mwilini
-
Utafiti2 days ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO