Connect with us

News

Damu imetapakaa kila mahali kwenye hizi hospitali:Casey

Avatar photo

Published

on

PICHA: Mvulana mwenye umri wa miaka 3, ambaye nyumba yake ilishambuliwa kwa bomu, anapata nafuu katika hospitali ya Nasser baada ya kukatwa sehemu ya mguu wake wa kulia.

Wahudumu wa afya huko Ukanda wa Gaza Jana jumanne wameendelea na kazi ya kuokoa maisha ya manusura wa mashambulio ya makambora yakiwemo mashambulio karibu na kambi ya wakimbizi kwenye eneo hilo lililozingirwa na Israel, mashambulio ambayo yameripotiwa kuua zaidi ya watu 100, limesema shirika la afya, WHO.

Mratibu wa Timu ya Matabibu wa Dharura Sean Casey amesema wagonjwa zaidi ya 100 walifikishwa Jumatatu kwenye hospitali ya Al-Aqsa ndani ya muda wa dakika 30, kufuatia milipuko karibu na kambi ya wakimbizi ya Al-Maghazi.

Wagonjwa wote hao walikuwa wanahitaji matibabu ya dharura wakiwa na majeraha makubwa,  amesema Afisa huyo wa WHO akizungumza na Idhaa ya Umoja wa Mataifa.

Amesema huku wagonjwa hao wakiletwa hospitali, takribani maiti wengine 100 walifikishwa muda huo huo.

Wamenasa chini  ya vifusi

Nayo Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya haki za binadamu, OHCHR, imeelezea wasiwasi wake mkubwa juu ya mashambulizi makubwa ya mabomu yanayoendelea kufanywa na jeshi la Israel katikati ya Gaza, ambapo zaidi ya mashambulizi 50 kutoka angani yameripotiwa kufanyika tangu tarehe 24 mwezi huu wa Desemba.

Mashambulio hayo yameripotiwa kuua zaidi ya wapalestina 100 tangu siku hiyo ambapo OHCHR inasema, “hii inatia zaidi wasiwasi kwa ripoti ya kwamba jeshi la Israel limeagiza wakazi walioko kusini mwa eneo la Wadi Gaza, wahamie eneo la kati la Gaza na Tal a-Sultan.”

Kambi tatu za wakimbizi zilipigwa kwa makombora, amesema msemaji wa OHCHR, Seif Magango kwenye taarifa iliyotolewa leo, akitaja kambi hizo kuwa ni Al Bureij, Al-Nuseirat na Al-Maghazi.

“Makombora mawili yalipiga makazi sav ana kuua tarkibani wapalestina 86 na kujeruhi wengine wengi,” amesema Magango huku akiongeza kuwa, “idadi isiyojulikana ya watu yaaminika wamefukiwa kwenye vifusi.”

Tedros achukizwa

Kupitia ukurasa wake kwenye mtandao wa X (zamani ukijulikana kama Twitter) Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus amelaani mauaji yanayosababishwa na mashambulizi ya kutoka angani yanayofanywa na jeshi la Israel dhidi ya Gaza ikiwa ni kisasi cha mashambulizi yaliyofanywa na Hamas tarehe 7 mwezi Oktoba mwaka huu. Takribani watu 1,200 waliuawa na wengine 240 walitekwa nyara siku hiyo.

“WHO ina wasiwasi mkubwa juu ya mzigo mkubwa kwa hospitali chache zinazoendelea kutoa huduma kwenye eneo hilo kutokana na kuendelezwa kwa chuki kati ya pande mbili hizo. Hospitali zilizosalia wazi ni chache ambapo nyingi zao uwezo wa kutoa huduma uko taabani,” alisema Dkt. Tedros siku ya Jumatatu.

Kupitia ukurasa wake wa X, Bwana Casey ameelezea hali katika hospitali ya Al-Aqsa kuwa ni dimbwi la damu. Alionesha Ahmed, mvulana mwenye umri wa miaka tisa ambaye alikuwa amalala kwenye sakafu ya hospitali hiyo baada ya kujeruhiwa kwa kiasi kikubwa na mlipuko wakati akivuka mtaa mmoja karibu na Nuseirat.

“Tumeona watoto, wanawake, vijana wa kiume, wazee wakivuja damu,” amesema Bwana Casey, huku akiongeza kuwa wagonjwa hawawezi kuhamishiwa eneo lingine kwa ajili ya matibabu ya kuokoa maisha yao.

“Damu imetapakaa kila mahali kwenye hizi hospitali. Tunaona wagonjwa wako na viwewe, damu kila mahali, tulishasema, ni mauaji.”

Shule ya Nuseirat iliyoko Gaza Kati inayoendeshwa na UNRWA sasa ni makazi ya maelfu ya watu waliofurushwa makwao kutokana na mashambulizi yanayoendelea Gaza.

Mapigano usiku kucha

“Hakuna mahali salama Gaza,” amesema Bwana Casey. “Hivi sasa hapa Rafah nje ya mlango wa jengo hili niliko, meta 50 hivi, kuna kambi ya maelfu ya watu ambao wamesaka hifadhi hapa. …wanaishi kwenye makazi yaliyofunikwa kwa karatasi za nailoni. Jana usiku tulisikia mashambulizi usiku kucha huku kukiwa na ripoti za kuweko kwa majeruhi wengi, wakipelekwa hospitali zilizoko hapa kusini.”

Uwezo wa hospitali Gaza hivi sasa ni takribani asilimia 20 ya kabla ya tarehe 7 Oktoba mashambulizi yalipoanza. “Takribani hospitali zote zimeacha kufanya kazi.”

Wanasubiri kufa

Bwana Casey amezungumzia pia wagonjwa walioko mahututi huko Gaza Kaskazini ambao kwa sasa wanasubiria kufa tu kwani hospitali ya mwisho iliyokuwa inatoa huduma imefungwa na sasa wako kwenye viwanja vya kanisa wakilala kwenye viti.

“Kiwango cha uharibifu ni kikubwa, barabara zimesheheni vifusi hivyo ni vigumu kufikia wahitaji.”

“Bado tunahitaji kuchukua hatua zaidi kusafirisha hawa wagonjwa, lakini fursa ya kufanya hivyo inazidi kuwa fingu kila uchao kwani ufikiaji wa hospitali ni mgumu,” amesema Bwana Casey.

Kwa mujibu wa Wizara ya Afya Gaza, takribani watu 20,000 yaaminika wameuawa tangu kuanza kwa mapigano Oktoba 7, mwaka huu.

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 months ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa3 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa3 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa5 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake5 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa4 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa3 hours ago

kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani

kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani Unapopata tatizo la kuharisha na kutapika kwa wakati mmoja unaweza kuwaza sana,...

Magonjwa2 days ago

Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu

Dalili za infection kwenye damu Mchafuko wa damu,chanzo,dalili na Tiba Mchafuko wa damu; hiki ni kiswahili ambacho watu wamezoea kukitumia...

Magonjwa5 days ago

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri Yapo magonjwa mbali mbali ya ngozi ambayo huweza kuathiri Sehemu za Siri za Mwanaume...

Magonjwa1 week ago

Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu

Dalili za acid reflux: Tatizo la Gastroesophageal reflux disease (GERD), ni tatizo ambalo huwapata Watu wengi,Tatizo hili hujulikana kwa jina...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe au ni ugonjwa ambao huhusisha ngozi kupoteza rangi...

Magonjwa4 weeks ago

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni,...

Magonjwa4 weeks ago

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu Utangulizi: Scabies huhusisha mtu kuwa na vipele na muwasho kwenye ngozi yake ambapo...

Magonjwa1 month ago

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume Gono ni neno maarufu ambalo kirefu chake ni Gonorrhea na kiswahili chake ni...

Magonjwa1 month ago

Dalili Mpya za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni Dalili za ukimwi kwenye ngozi Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala...

Magonjwa1 month ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Trending