Events
Raia wa Togo ni miongoni mwa watu waliokuwemo katika ajali ARUSHA
Raia wa Togo ni miongoni mwa watu waliokuwemo katika ajali iliyotokea Februari 25. 2024 katika eneo la Ngaramtoni mkoani Arusha
na kusababisha vifo vya watu 25 na wengine zaidi ya 20 kujeruhiwa.
Kwa sasa Apelo anapatiwa matibabu katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Arusha, Mount Meru ambapo ameishukuru Serikali kwa huduma nzuri za matibabu anazopatiwa hospitalini hapo.
Amesema kwa namna ajali hiyo ilivyokuwa na huduma alizopatiwa kama asingekuwa Tanzania angekuwa amekwishafariki dunia na kwamba ukarimu wa Watanzania ndio uliookoa maisha yake.
“Kwa ajali hii ningekuwa nchini kwetu tayari ningekuwa nimepoteza maisha, kwani kule bila kulipia huduma za matibabu hupatiwi huduma, lakini kwa Tanzania walivyo wakarimu na weledi wameweza kuokoa maisha yangu mpaka sasa naendelea vizuri na naweza kuongea,” Amesema raia huyo wa Togo
Apelo alikuja Tanzania kushiriki kwenye semina iliyokuwa ikifanyika mkoani Arusha, ambapo pia walikwenda kufanya utalii na walipokuwa wakirejea ndipo wakapata ajali.
-
Uzazi/Ujauzito6 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Uzazi/Ujauzito4 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa5 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Magonjwa3 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events7 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News5 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
afyatips19 hours ago
Madhara ya damu kuwa nyingi mwilini
-
Utafiti2 days ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO