News
Israel Yaomboleza Vifo Vya Mateka Wa Israel Waliouawa Kimakosa Na Jeshi Lake
Israel Yaomboleza Vifo Vya Mateka Wa Israel Waliouawa Kimakosa Na Jeshi Lake
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, ameyataja mauaji ya mateka hao kuwa ni “janga lisilovumilika” na kuahidi kuendelea “kwa juhudi kubwa za kuwarejesha mateka wote nyumbani wakiwa salama”.
Israel inaomboleza vifo vya mateka watatu wa Israel waliouawa kimakosa na wanajeshi wa Israel wakati wa operesheni yake ya ardhini katika Ukanda wa Gaza.
Msemaji mkuu wa jeshi hilo, Admirali Daniel Hagari, amesema vikosi vya Israel viliwatambua kimakosa mateka hao kama tishio, na kuwafyatulia risasi Ijumaa. Alisema kuwa haijafahamika iwapo mateka hao waliwatoroka watekaji wao, au walikuwa wametelekezwa.
Vifo vyao vilitokea katika eneo la Shijaiyah huko Gaza City, eneo la mapigano ya umwagaji damu kati ya jeshi la Israel na wanamgambo wa Hamas. Alisema jeshi limeelezea masikitiko makubwa na linafanya uchunguzi.
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, ameyataja mauaji ya mateka hao kuwa ni “janga lisilovumilika” na kuahidi kuendelea “kwa juhudi kubwa za kuwarejesha mateka wote nyumbani wakiwa salama”.
-
Uzazi/Ujauzito6 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Uzazi/Ujauzito4 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa5 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Magonjwa3 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events7 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News5 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
afyatips18 hours ago
Madhara ya damu kuwa nyingi mwilini
-
Utafiti2 days ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO