News
Nyota wa soka wa Uhispania Jenni Hermoso afunguka kuhusu jinsia yake
Nyota wa soka wa Uhispania Jenni Hermoso afunguka kuhusu jinsia yake, anasema ni ‘rahisi zaidi’ kujitokeza katika mchezo wa wanawake kuliko wa wanaume.
Nyota wa soka wa Uhispania, Jenni Hermoso amefunguka kuhusu jinsia yake na jinsi ilivyo ‘rahisi zaidi’ kujitokeza katika mchezo wa wanawake kuliko wa wanaume,
Hermoso amekuwa kwenye vichwa vya habari mwaka jana baada ya rais wa zamani wa Uhispania Luis Rubiales kumbusu midomoni bila ridhaa yake kufuatia ushindi wao wa fainali ya Kombe la Dunia dhidi ya England katika kashfa iliyotikisa soka.
Fowadi huyo mwenye umri wa miaka 33 baadaye alijitokeza kukashifu busu hilo na kusaidia kukuza vuguvugu la ‘Me Too’ nchini. Sasa ameamua kuzungumzia jinsia yake.
Hermoso, ambaye hakuwahi kujadili suala hilo na familia yake akikua, alisema ilikuwa rahisi zaidi kukumbatia, kujitokeza kama mwanasoka wa kike kabla ya kukiri kwamba wanasoka wa kiume wanakabiliwa na mapambano makubwa zaidi.
“Sijawahi kuwaambia wazazi wangu waziwazi kwamba napenda wasichana,” aliambia kipindi cha TV cha Uhispania Planeta Calleja. “Ni jambo ambalo siku zote limekuwa mwiko, lakini kwa kweli hakukuwa na haja ya kulijadili kwa uwazi: watu walionizunguka walijua. Wazazi wangu pia hawakuwa wajinga.
‘Sikuzote nimekuwa nikizungumza wazi na mama yangu, lakini nilipopata shida, nilimgeukia shangazi yangu Carol, ambaye alikuwa msiri wangu.
‘Kwenye soka la wanawake ni rahisi zaidi kutoka kuliko katika soka ya wanaume.
‘Kuna baadhi ya wanasoka wa kiume wamejitokeza, lakini wamekutana na chuki nyingi. Wanasoka wa kiume hawana nia ya kulizungumzia kwa sababu wanatendewa tofauti.’
Akizungumzia maisha yake ya mapenzi, Hermoso, ambaye kwa sasa hajaoa alisema kwa sasa amepata ‘utulivu’ katika maisha yake baada ya hapo awali kuruhusu maisha yake ya kibinafsi kuzuiwa na uchezaji wake uwanjani.
“Nimekuwa katika mapenzi, lakini si sasa hivi,” aliongeza. ‘Ni moja ya mambo bora nimegundua: jinsi ya kuishi kama mimi mwenyewe.
‘Maisha yangu ya kibinafsi na maisha yangu kama mchezaji wa soka yamekuwa yakihusishwa kwa karibu. Ikiwa ningekuwa na matatizo, soka langu lingekuwa janga. Inaweza kuwa mbaya Zaidi, haswa ikiwa moyo wangu ulivunjika. Sasa kwa bahati nzuri nimepata utulivu.’
Majadiliano ya wazi ya Hermoso kuhusu maisha yake ya kibinafsi yanakuja katikati ya kashfa yake inayoendelea ya ‘kiss-gate’.
-
Uzazi/Ujauzito5 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Magonjwa4 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Uzazi/Ujauzito3 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa7 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Magonjwa2 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events6 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News4 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
Utafiti23 hours ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO