News
Mpaka Sasa Mikoa Sita ya Tanzania ina kipindupindu
![](https://afyaclass.com/mk_omb/uploads/2024/01/images-7.jpeg)
Mpaka Sasa Mikoa Sita ya Tanzania ina kipindupindu.
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu ametoa taarifa ya hali ya utoaji huduma za afya nchini kwa mwaka 2023 katika mkutano wake na Waandishi wa Habari Jijini Dar es salaam ambapo pamoja na mambo mengine amesema mpaka sasa kuna Mikoa sita ambayo inaendelea na mlipuko wa kipindupindu nchini.
Waziri Ummy amenukuliwa akisema “kwa mwaka jana 2023 mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu ulitolewa taarifa katoka Mikoa 12 nchini ambapo Wagonjwa 927 na vifo 27 vilitolewa taarifa, Mkoa wa Arusha uliongoza kwa visa 214 lakini bahati nzuri hakukutokea kifo, katika Mkoa wa Mara jumla ya visa 193 na vifo vinane (8) vilitolewa taarifa, Mkoa wa Simiyu Visa 184 na vifo Viwili (2)”
“Mpaka sasa kuna Mikoa 6 ambayo inaendelea na mlipuko ambayo ni Shinyanga, Ruvuma, Tabora, Simiyu, Mwanza na Kagera”
Waziri Ummy amewapongeza Wakuu wa Mikoa pamoja na watendaji wa Sekta ya Afya ngazi ya Mikoa na Halmashauri kwa kuendelea kuimarisha usimamizi ili ugonjwa huo udhibitiwe.
-
Magonjwa4 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Elimu&Ushauri6 days ago
Afya za watu bilioni 1.8 duniani matatani kwa kutokufanya Mazoezi – WHO
-
Uzazi/Ujauzito2 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Magonjwa1 day ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Events3 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News6 days ago
Mlipuko Mbaya wa homa ya nyani watokea tena KIVU KASKAZINI
-
Uzazi/Ujauzito10 hours ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
News2 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani