News
Upatikanaji wa maji safi na salama kupunguza magonjwa ya mlipuko
![](https://afyaclass.com/mk_omb/uploads/2024/02/images-4-3.jpeg)
Upatikanaji wa maji safi na salama kupunguza magonjwa ya mlipuko
Na WAF – Simiyu
Wizara ya Afya, Wakala wa Nishati Vijijini (REA), kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU), kwa pamoja kupitia mradi wa kupambana na Magonjwa ya Mlipuko wamewezesha vijiji vya Nyanguge na Bunamhala Wilayani Bariadi, Mkoani Simiyu, kufikiwa na huduma ya maji safi na salama.
Kupitia mradi huo Visima vimekarabatiwa na kuwekwa pampu za umeme na kuwezesha upatikanaji wa maji safi na salama mabadiliko ambayo yameleta furaha kwa wananchi kwa kuchochea ustawi wa afya na kupunguza hatari ya magonjwa ya mlipuko.
Mwenyekiti wa kamati ya maji katika Wilaya ya Bariadi, Swales Ngusa, amesema kuboreshwa kwa ubora wa maji kumechochewa na gharama za uendeshaji kupungua kufuatia upatikanaji wa umeme.
Kwa upande wake, Afisa Afya na Mratibu wa Elimu ya Afya kwa Umma Mkoani Simiyu, Bashiri Salum, amethibitisha kuwa matumizi ya dawa ya Klorini yamekuwa muhimu katika kuhakikisha maji yanakuwa safi na salama.
Mradi huo unaotekelezwa katika wilaya kadhaa za Mkoa wa Simiyu unalenga kuhakikisha upatikanaji wa umeme vijijini na kuwezesha huduma za maji safi na salama, huku ikilenga kuboresha afya na ustawi wa jamii awali wananchi walikabiliwa na changamoto za kuchota maji katika vyanzo visivyokuwa salama, hali iliyosababisha kuongezeka kwa magonjwa ya mlipuko kama vile Kipindupindu.
-
Magonjwa4 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Elimu&Ushauri6 days ago
Afya za watu bilioni 1.8 duniani matatani kwa kutokufanya Mazoezi – WHO
-
Uzazi/Ujauzito2 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Magonjwa1 day ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Events3 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News6 days ago
Mlipuko Mbaya wa homa ya nyani watokea tena KIVU KASKAZINI
-
Uzazi/Ujauzito10 hours ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
News2 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani